1 Wafalme 14 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Kifo cha mwana wa Yeroboamu

1Wakati ule, Abiya mwana wa mufalme Yeroboamu, akagonjwa.

2Yeroboamu akamwambia muke wake: “Ujigeuze kusudi watu wasitambue kwamba wewe ni muke wangu, uende Shilo kwa nabii Ahiya aliyesema kwamba mimi nitakuwa mufalme wa Israeli.

3Umupelekee mikate kumi, na maandazi, na chupa moja ya asali. Yeye atakuambia yatakayomupata mutoto wetu.”

4Basi, muke wa Yeroboamu akaondoka, akaenda Shilo kwa Ahiya. Wakati ule, Ahiya alikuwa hawezi tena kuona sawasawa kwa sababu ya uzee.

5Yawe alikuwa amekwisha kumwambia Ahiya kwamba muke wa Yeroboamu alikuwa katika njia, anakuja kumwuliza yatakayomupata mwana wake mugonjwa, na jinsi atakavyomujibu.

Muke wa Yeroboamu alipofika, alijisingizia kuwa mutu mwingine.

6Lakini Ahiya alipomusikia anaingia kwenye mulango, alisema: “Karibu ndani muke wa Yeroboamu. Lakini mbona unajigeuza kuwa mutu mwingine? Niko na ujumbe usiokuwa muzuri kwako!

7Kwenda umwambie Yeroboamu kwamba Yawe, Mungu wa Israeli, anasema hivi: ‘Nilikuchagua kati ya watu, nikakufanya kiongozi wa watu wangu Waisraeli,

8nikaunyanganya ufalme utoke kwa wazao wa Daudi, nikakupa wewe. Lakini wewe ni kinyume kabisa cha mutumishi wangu Daudi ambaye alizishika amri zangu. Alifuata mapenzi yangu kwa moyo wake wote na kutenda tu yanayokuwa sawa mbele ya macho yangu.

9Wewe umetenda uovu mubaya zaidi kuliko waliotenda wale waliokutangulia. Wewe umenikasirikisha kwa kujitengenezea miungu mingine na sanamu za kufua, kisha umeniacha.

10Basi, sasa nitailetea jamaa hii ya Yeroboamu hasara, nitawaua wanaume wote wa jamaa yake katika Israeli, akuwe mutumwa au huru. Watu wa jamaa yake wote nitawateketeza kama vile mutu anavyoteketeza mavi, mpaka yatoweke.

11Mutu yeyote wa jamaa ya Yeroboamu atakayekufia katika muji, imbwa watamukula; na yeyote atakayekufia katika shamba, ndege watamukula.’ Yawe amesema hivyo.”

12Ahiya akamwambia muke wa Yeroboamu: “Simama, urudie kwako sasa. Mara tu utakapoingia katika muji, mwana wako atakufa.

13Watu wote wa Israeli watafanya kilio na kumuzika. Lakini, ni huyo tu wa jamaa ya Yeroboamu atakayezikwa, maana ni yeye tu wa jamaa ya Yeroboamu aliyepata kupendezwa na Yawe, Mungu wa Israeli.

14Tena leo hii, Yawe ataweka mufalme mwingine katika Israeli ambaye ataua watu wa jamaa ya Yeroboamu.

15Hakika, tangu sasa, Yawe atawapiga watu wa Israeli, nao watatikisika kama unyasi unavyotikiswa ndani ya muto. Atawaongoa kutoka inchi hii nzuri aliyowapa babu zao, na kuwatawanya mbali, ngambo ya muto Furati, kwa sababu wamemukasirikisha Yawe kwa kujitengenezea sanamu za Ashera.

16Yawe ataitupilia Israeli kwa sababu ya zambi za Yeroboamu ambaye alitenda zambi na kuwasukuma watu wa Israeli vilevile watende zambi.”

17Halafu, muke wa Yeroboamu akaondoka, akashika safari mpaka Tirza. Mara tu alipofika kwenye mulango, mutoto akakufa.

18Watu wote wa Israeli wakamuzika na kufanya kilio kama vile Yawe alivyosema, kwa njia ya nabii Ahiya, mutumishi wake.

Kifo cha Yeroboamu

19Matendo mengine ya mufalme Yeroboamu, jinsi alivyopigana vita na alivyotawala, yote yameandikwa katika Kitabu cha Mambo ya Siku za Wafalme wa Israeli.

20Yeroboamu alitawala kwa muda wa miaka makumi mbili na mbili, halafu akakufa, na mwana wake Nadabu akatawala kwa pahali pake.

Mufalme Rehoboamu wa Yuda(2 Sik 13.1–14.1)

21Rehoboamu mwana wa Solomono alikuwa na umri wa miaka makumi ine na mumoja alipoanza kutawala inchi ya Yuda. Naye alitawala kwa muda wa miaka kumi na saba katika Yerusalema, muji ambao Yawe aliuchagua kati ya miji ya makabila yote ya Israeli kusudi aabudiwe humo. Mama ya Rehoboamu jina lake lilikuwa Nama kutoka kabila la Waamoni.

22Watu wa Yuda walitenda maovu mbele ya Yawe. Walimukasirikisha kwa zambi zao walizotenda, nyingi kuliko za babu zao.

23Walijitengenezea vilevile pahali pa ibada, minara ya kutambikia, na sanamu za Ashera, juu ya kila kilima kirefu na chini ya kila muti wenye majani mengi.

24Kukakuwa hata ibada za uasherati katika inchi, nao walitenda matendo ya kuchukiza, sawasawa na yale matendo ya mataifa ambayo Mungu aliyafukuza mbele ya Waisraeli.

25Katika mwaka wa tano wa utawala wa Rehoboamu, Sisaki mufalme wa Misri aliushambulia Yerusalema.

26Akaitwaa hazina yote ya nyumba ya Yawe na ya nyumba ya kifalme. Alitwaa kila kitu; naye alitwaa ngao zote za zahabu Solomono alizozitengeneza.

27Pahali pa ngao hizo, mufalme Rehoboamu alitengeneza ngao za shaba na kuziweka chini ya ulinzi wa wachungaji wa mulango wa nyumba ya kifalme.

28Kila wakati mufalme alipokwenda katika nyumba ya Yawe, walinzi walizibeba ngao hizo, na nyuma walizirudisha katika chumba cha ulinzi.

29Mambo mengine ya Rehoboamu na yote aliyofanya yameandikwa katika Kitabu cha Mambo ya Siku za Wafalme wa Yuda.

30Siku zote kulikuwa vita kati ya Rehoboamu na Yeroboamu.

31Nyuma, Rehoboamu alikufa na kuzikwa kwenye makaburi ya wazee wake, katika muji wa Daudi. Mama yake aliitwa Nama kutoka katika kabila la Waamoni, na mwana wake Abiyamu akatawala kwa pahali pake.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help