Kumbukumbu la Sheria 8 - Swahili Congo Revised Bible 2002

1“Mutakuwa waangalifu kwa kutenda amri zote ninazowapa leo, kusudi mupate kuishi na kuongezeka, na muingie na kuirizi inchi ile ambayo Yawe aliapa kuwapa babu zenu.

2Mukumbuke jinsi Yawe, Mungu wenu, alivyowaongoza katika safari ndefu kupitia katika jangwa kwa muda wa miaka hiyo makumi ine, kusudi awanyenyekeze na kuwajaribu kusudi ajue yanayokuwa ndani ya mioyo yenu, na kama mungeshika amri zake au hapana.

3Aliwazarau akawaacha muone njaa na kisha akawapa mana mukule, chakula ambacho hamukukijua, wala babu zenu hawajapata kukijua. Alifanya hivyo kusudi apate kuwafundisha kwamba mwanadamu haishi kwa mukate tu, lakini kwa kila neno Yawe analosema.

4Wakati huo wa miaka makumi ine nguo zenu hazikuchakaa, wala miguu yenu haikuvimba.

5Mukumbuke kwamba Yawe, Mungu wenu, anawaazibu kama vile baba anavyoazibu mwana wake.

6Hivyo, mushike amri za Yawe, Mungu wenu, mupate kufuata njia zake na kumwogopa yeye.

7Yawe, Mungu wenu, anawaleta kwenye inchi nzuri, inchi yenye vijito na chemichemi, na maji yanayobubujika kutoka bonde na milima;

8inchi yenye ngano na shayiri, mizabibu, mitini, mikomamanga, mizeituni na asali.

9Huko mutapata chakula tele na hamutapungukiwa kitu. Mawe yake yana chuma, na kwenye milima yake munaweza kuchimba shaba.

10Mutakula na kushiba, mutamushukuru Yawe, Mungu wenu, kwa inchi nzuri aliyowapa.

Onyo juu ya kumusahau Yawe

11“Muhakikishe kwamba hamutamusahau Yawe, Mungu wenu, kwa kutoshika amri zake, maagizo yake na masharti yake ninayowaamuru leo.

12Mukisha kula na kushiba, kujijengea nyumba nzuri na kuishi humo,

13na wakati ambapo ngombe na kondoo wenu, zahabu na feza yenu, na kila kitu munachokuwa nacho kitakuwa kimeongezeka,

14musikuwe na kiburi na kumusahau Yawe, Mungu wenu, aliyewatoa katika inchi ya Misri, pahali mulipokuwa watumwa.

15Ni yeye aliyewaongoza katika lile jangwa kubwa na la kutisha, lenye nyoka wenye sumu na nge katika inchi ile yenye kukauka isiyokuwa na maji, aliwatolea maji kutoka kwenye jiwe gumu.

16Tena ni yeye aliyewakulisha mana katika jangwa, chakula ambacho babu zenu hawajapata kukijua. Alifanya hayo yote kusudi awanyenyekeze na kuwajaribu kwa kuwapima apate kuwajalia mema kwa mwisho.

17Hivyo mufanye angalisho kusudi musijisemeshe ndani ya mioyo yenu: ‘Tumejitajirisha kwa uwezo na nguvu zetu wenyewe’.

18Mukumbuke kwamba Yawe, Mungu wenu, ndiye anayewapa uwezo wa kupata utajiri. Anafanya hivyo kwa kuimarisha agano alilofanya na babu zenu mpaka leo.

19Lakini mukimusahau Yawe, Mungu wenu, na kufuata miungu mingine kwa kuitumikia na kuiabudu, ninawaonya vikali leo hii kwamba hakika mutaangamia.

20Musipomutii Yawe, mutaangamia kama vile mataifa ambayo anayaangamiza mbele yenu.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help