1Haleluia!
Mumushukuru Yawe kwa sababu ni muzuri!
Wema wake unadumu milele!
2Ni nani anayeweza kutaja matendo ya Yawe?
Ni nani anayeweza kumusifu kama anavyostahili?
3Heri wale wanaofuata sheria ya Mungu,
wanaotenda siku zote mambo ya haki.
4Unikumbuke, ee Yawe,
unapowaonyesha watu wako upendo.
Unisaidie wakati unapowaokoa,
5kusudi niweze kuona uheri wa wachaguliwa wako,
nipate kushiriki katika furaha ya taifa lako,
na kuona utukufu pamoja na watu wako.
6Tumetenda zambi sisi na babu zetu;
tumetenda maovu, tumefanya mabaya.
7Babu zetu walipokuwa Misri,
hawakujali matendo ya ajabu ya Mungu;
hawakukumbuka wingi wa wema wake,
lakini walimwasi kando ya bahari Nyekundu.
8Hata hivyo Mungu aliwaokoa kama alivyoahidi,
kusudi aonyeshe nguvu yake kubwa.
9Alikaripia bahari Nyekundu, ikakauka;
akawapitisha humo kama katika inchi kavu.
10Aliwaokoa katika mikono ya waliowachukia;
aliwaokoa kutoka nguvu za waadui zao.
11Maji ya bahari yaliwafunika waadui zao;
wala hapakubakia hata mumoja wao.
12Hapo watu wake wakaamini maneno yake,
wakamwimbia nyimbo za sifa yake.
13Lakini bila kukawia walisahau matendo yake,
wakaacha kutegemea shauri lake.
14Walipatwa na tamaa kubwa kule katika jangwa,
wakamupima Mungu kule kwenye ukiwa.
15Naye akawapa kile walichoomba,
lakini akaleta magonjwa makali kati yao.
16Kule katika kambi walimwonea Musa wivu,
na Haruni, mutumishi mutakatifu wa Yawe.
17Halafu udongo ukafunguka ukamumeza Datani,
na kumuzika Abiramu na kundi lake lote;
18moto ukawatokea wafuasi wao,
ukawateketeza watu hao waovu.
19Walitengeneza mwana-ngombe wa zahabu kule Horebu,
wakaabudu sanamu hiyo ya chuma;
20walibadilisha utukufu wa Mungu
kwa sanamu ya nyama ambaye anakula majani.
21Walimusahau Mungu aliyewaokoa,
aliyetenda mambo makubwa katika inchi ya Misri,
22maajabu katika inchi hiyo ya Hamu,
na mambo ya kutisha katika bahari Nyekundu.
23Mungu alisema atawaangamiza watu wake,
lakini Musa, muchaguliwa wake, aliingilia kati,
akazuia hasira yake isiwaangamize.
24Kisha wakazarau inchi ile ya kupendeza,
kwa sababu hawakuaminia ahadi ya Mungu.
25Walinungunika ndani ya hema zao,
wala hawakumusikiliza Yawe.
26Hivyo Mungu akainua mukono, akaapa
kwamba atawaangamizia katika jangwa,
27atawatawanya wazao wao kati ya watu,
na kuwasambaza katika dunia yote.
28Kisha wakajiunga kumwabudu Bali kule Peori,
wakakula sadaka zilizotambikiwa kwa mizimu.
29Waliichochea hasira ya Yawe kwa matendo yao,
magonjwa makali yakatokea kati yao.
30Lakini Finehasi akasimama kutoa malipizi,
na yale magonjwa yakakoma.
31Jambo hilo linakumbukwa kwa heshima yake,
tangu wakati huo na nyakati zote.
32Walimukasirikisha Mungu penye maji ya Meriba.
Musa akapata taabu kwa ajili yao.
33Walimuletea uchungu katika roho,
hata akasema maneno bila kufikiri.
34Hawakuwaua watu wa mataifa
kama vile Yawe alivyowaamuru.
35Lakini walichanganyika na watu wa mataifa,
wakajifunza kutenda mambo yao.
36Waliabudu sanamu za miungu yao,
nazo zikakuwa mutego wa kuwaangamiza.
37Waliua watoto wao wanaume na wabinti,
wakawatoa sadaka kwa mapepo.
38Walimwanga damu ya wasiokuwa na kosa,
damu ya watoto wao wanaume na wabinti
ambao waliwatoa sadaka kwa sanamu za Wakanana,
nayo inchi ikachafuliwa kwa uuaji huo.
39Hivyo wakajichafua kwa matendo yao,
wakakosa uaminifu kwa Mungu kama wazini.
40Hasira ya Yawe ikawawakia watu wake,
akachukizwa sana na hao waliokuwa mali yake.
41Akawatoa katika mikono ya watu wa mataifa,
hao wenye kuwachukia, wakawatawala.
42Waadui zao waliwagandamiza,
wakawatumikisha kwa nguvu.
43Mara nyingi Mungu aliwaokoa watu wake,
lakini wao wakachagua kumwasi,
wakazidi kuzama katika uovu wao.
44Hata hivyo Mungu aliona taabu yao,
wakati aliposikia kilio chao;
45kwa ajili yao alilikumbuka agano lake,
akawahurumia kwa wingi wa wema wake.
46Aliwafanya wale waliowaangamiza wawaonee huruma.
47Utuokoe, ee Yawe, Mungu wetu,
utukusanye pamoja kutoka kwa mataifa,
tupate kusifu jina lako takatifu,
na kuona utukufu juu ya sifa zako.
48Yawe, Mungu wa Israeli, asifiwe
tangu milele na hata milele!
Na watu wote waseme: “Amina!”
Haleluia!
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.