Zaburi 99 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Mungu ni mutawala mukubwa

1Yawe anatawala,

mataifa yanatetemeka!

Ameikaa juu ya makerubi,

nayo dunia inatikisika!

2Yawe ni mukubwa katika Sayuni;

ametukuzwa kuliko mataifa yote.

3Wote wasifu jina lake kubwa la kutisha.

Yeye ni mutakatifu!

4Ee mufalme mukubwa, mupenda haki,

umesimamisha usawa katika Israeli;

umeleta sheria na haki.

5Mumusifu Yawe, Mungu wetu;

muiname uso mpaka chini mbele yake.

Yeye ni mutakatifu!

6Musa na Haruni walikuwa makuhani wake;

Samweli alikuwa kati ya waliomulilia.

Walimulilia Yawe naye akawasikiliza.

7Alisema nao katika nguzo ya wingu;

walitimiza maagizo yake na masharti aliyowapa.

8Ee Yawe, Mungu wetu, wewe uliwasikiliza;

ulikuwa kwao Mungu mwenye kusamehe,

ingawa uliwaazibu kwa makosa yao.

9Mumusifu Yawe, Mungu wetu;

muiname kwa mulima wake mutakatifu!

Yawe, Mungu wetu, ni mutakatifu.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help