1Yawe anatawala,
mataifa yanatetemeka!
Ameikaa juu ya makerubi,
nayo dunia inatikisika!
2Yawe ni mukubwa katika Sayuni;
ametukuzwa kuliko mataifa yote.
3Wote wasifu jina lake kubwa la kutisha.
Yeye ni mutakatifu!
4Ee mufalme mukubwa, mupenda haki,
umesimamisha usawa katika Israeli;
umeleta sheria na haki.
5Mumusifu Yawe, Mungu wetu;
muiname uso mpaka chini mbele yake.
Yeye ni mutakatifu!
6Musa na Haruni walikuwa makuhani wake;
Samweli alikuwa kati ya waliomulilia.
Walimulilia Yawe naye akawasikiliza.
7Alisema nao katika nguzo ya wingu;
walitimiza maagizo yake na masharti aliyowapa.
8Ee Yawe, Mungu wetu, wewe uliwasikiliza;
ulikuwa kwao Mungu mwenye kusamehe,
ingawa uliwaazibu kwa makosa yao.
9Mumusifu Yawe, Mungu wetu;
muiname kwa mulima wake mutakatifu!
Yawe, Mungu wetu, ni mutakatifu.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.