1Lakini Waisraeli hawakukuwa waaminifu juu ya vile vitu vilivyotolewa viangamizwe maana Akana mwana wa Karmi, mujukuu wa Zabedi, wa ukoo wa Zera, wa kabila la Yuda, alitwaa vimoja kati ya vitu vilivyoamriwa viteketezwe. Kwa hiyo hasira ya Yawe ikawaka juu ya Waisraeli.
2Yoshua akawatuma watu kutoka Yeriko kwenda muji wa Ai, unaokuwa karibu ya Beti-Aweni, upande wa mashariki wa Beteli, akawaambia: “Mwende muipeleleze inchi.” Nao wakaenda na kuupeleleza muji wa Ai.
3Waliporudi, wakamwambia Yoshua: “Hakuna lazima ya kupeleka watu wote kuushambulia muji wa Ai, maana wakaaji wake ni wachache tu. Watu elfu mbili au tatu watatosha.”
4Basi, watu kama elfu tatu hivi wakaenda kuushambulia muji wa Ai, lakini wakakimbizwa na wakaaji wa muji huo.
5Watu wa Ai wakawaua Waisraeli makumi tatu na sita na kuwafukuza wengine kutoka mulango wa muji mpaka Sebarimu, wakawaua kwenye muteremuko. Waisraeli wakavunjika moyo na kuregea kama maji.
6Yoshua akapasua nguo yake, yeye pamoja na wazee wa Israeli. Wakajitupa chini ya Sanduku la Yawe mpaka magaribi; wakajitia mavumbi juu ya vichwa vyao.
7Yoshua akasema: “Ole wetu, ee Bwana wetu Yawe! Kwa nini umetuvukisha muto Yordani kwa kututia katika mikono ya Waamori kusudi watuangamize? Tungalifurahi kubaki ngambo ya muto Yordani!
8Ee Bwana, niseme nini wakati Waisraeli wamewakimbia waadui zao?
9Basi, Wakanana pamoja na wakaaji wote wa inchi hii watakapopata habari hiyo watatuzunguka na kutufuta kabisa katika dunia. Sasa utafanya nini kwa kuonyesha ukubwa wa jina lako?”
10Yawe akamwambia Yoshua: “Simama! Mbona umejitupa chini hivyo?
11Waisraeli wametenda zambi, maana wamelivunja agano langu nililowaamuru washike. Wametwaa vimoja kati ya vitu vilivyotolewa viangamizwe. Wameviiba na kudanganya, wakaviweka pamoja na vitu vyao.
12Kwa hiyo Waisraeli hawawezi kuwashinda waadui zao. Wanawakimbia waadui zao kwa sababu wamejifanya wenyewe kuwa kitu cha kuangamizwa! Sitakuwa pamoja nao tena musipoharibu vitu vinavyokuwa kati yenu vilivyotolewa viangamizwe.
13Basi, simama uwatakase watu, uwaambie wajitakase na kujitayarisha kwa siku ya kesho, maana mimi Yawe, Mungu wa Israeli, ninasema hivi: ‘Kati yenu kuna vitu vilivyotolewa viangamizwe. Hamuwezi kuwashinda waadui zenu mpaka vitu hivyo vimeondolewa kati yenu!
14Kwa hiyo kesho asubui wote mutakuja mbele yangu, kabila kwa kabila. Kabila nitakalolichagua litakwenda mbele, ukoo kwa ukoo. Ukoo nitakaouchagua utakwenda mbele, jamaa kwa jamaa. Na jamaa nitakayoichagua itakwenda mbele, mutu mumoja mumoja.
15Mutu yeyote atakayepatikana akiwa na vitu vilivyotolewa viangamizwe atateketezwa kwa moto, yeye pamoja na kila kitu chake maana ameliasi agano langu mimi Yawe, akatenda jambo la haya katika Israeli.’ ”
16Basi, Yoshua akaamuka asubui mapema, akawaleta Waisraeli wote karibu, kabila kwa kabila. Kabila la Yuda likachaguliwa.
17Akazileta karibu ukoo za Yuda, ukoo kwa ukoo; na ukoo wa Zera ukachaguliwa. Akazileta karibu jamaa za ukoo wa Zera, jamaa kwa jamaa; na jamaa ya Zabedi ikachaguliwa.
18Yoshua akaileta jamaa ya Zabedi karibu, nyumba kwa nyumba; na nyumba ya Akana mwana wa Karmi, mujukuu wa Zabedi mwana wa Zera, wa kabila la Yuda, ikachaguliwa.
19Yoshua akamwambia Akana: “Mwana wangu, umutukuze Yawe, Mungu wa Israeli, umusifu na kisha uniambie yale uliyotenda, wala usinifiche.”
20Akana akamujibu: “Ni kweli nimetenda zambi mbele ya Yawe, Mungu wa Israeli. Na hivi ndivyo nilivyofanya:
21Nilipoona vazi moja zuri kutoka Sinari kati ya vitu tulivyonyanganya, vikoroti mia mbili vya feza na furushi ya zahabu yenye uzito wa vikoroti makumi tano vya feza, nikavitamani na kuvitwaa; nikavificha katika udongo ndani ya hema langu; na feza iko chini ya vitu hivyo.”
22Basi, Yoshua akawatuma wajumbe, nao wakakimbia kwenye hema kwa Akana. Na kumbe, vitu vilikuwa vimefichwa katika hema na feza ikiwa chini yake.
23Wakavitwaa toka katika hema na kuvipeleka kwa Yoshua na watu wote wa Israeli; nao wakaviweka chini, mbele ya Yawe.
24Yoshua pamoja na Waisraeli wote, wakamukamata Akana mwana wa Zera, pamoja na feza, nguo, zahabu, watoto wake wa kiume na wabinti zake, ngombe, punda na kondoo wake, hema lake na kila kitu alichokuwa nacho na kuwapeleka kwenye bonde la Akori.
25Yoshua akamwuliza Akana: “Kwa nini umetuletea taabu? Yawe atakuletea taabu wewe mwenyewe leo.” Waisraeli wote wakamupiga Akana kwa mawe mpaka akakufa. Kisha wakawapiga jamaa yake yote kwa mawe mpaka wakakufa, wakawateketeza wote kwa moto.
26Halafu wakalundika mawe mengi juu yake, ambayo yako mpaka leo. Hapo hasira ya Yawe ikapoa; na pahali pale pakaitwa Bonde la Akori, ni kusema Bonde la Taabu, mpaka hivi leo.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.