1 Samweli 10 - Swahili Congo Revised Bible 2002

1Halafu Samweli akatwaa chupa ndogo ya mafuta akamumiminia Saulo juu ya kichwa, akamubusu na kumwambia: “Yawe amekutia mafuta ukuwe mutawala juu ya watu wake.

2Leo tutakapoagana, utakutana na watu wawili karibu na kaburi la Rakeli kule Zeleza katika inchi ya Benjamina. Hao watakuambia kwamba wale punda uliokuwa unawatafuta wamekwisha kupatikana. Baba yako ameacha kufikiri juu ya punda, lakini ana wasiwasi juu yako, akijiuliza kila mara: ‘Nitafanya nini juu ya mwana wangu?’

3Kutoka pale utakwenda kwenye muti wa mwalo wa Tabori, pahali ambapo utakutana na wanaume watatu wakiwa katika njia kwenda kumutolea Mungu sadaka, kule Beteli. Mumoja wao atakuwa akipeleka wana-mbuzi watatu, wa pili atakuwa akipeleka mikate mitatu na wa tatu atakuwa akibeba karabia ya divai.

4“Watakusalimia na kukupa mikate miwili, nawe utaipokea toka katika mikono yao.

5Kisha, utafika kule Gibeati-Elohimu, pahali ambapo pana kambi ya waaskari wa Wafilistini. Pale, utakapokuwa unakaribia muji, utakutana na kundi la manabii. Manabii hao watakuwa wanatoka kwenye nafasi ya kuabudia na wakipiga vinubi, matari, filimbi na zeze, na watakuwa wanatabiri.

6Roho wa Yawe atakufikia kwa nguvu, nawe utaanza kutabiri pamoja nao na kugeuka kuwa mutu mwingine.

7Wakati mambo haya yatakapokutokea, chochote utakachoweza kufanya ukifanye, maana Mungu yuko pamoja nawe.

8Utanitangulia kwenda Gilgali, pahali ambapo nitakukuta na kutoa sadaka ya kuteketezwa na sadaka za amani. Utaningojea pale kwa muda wa siku saba mpaka nikuje na kukuonyesha la kufanya.”

9Saulo alipogeuka kwa kumwacha Samweli, Mungu akabadilisha moyo wa Saulo. Yale yote aliyoambiwa na Samweli yakatokea siku hiyo.

10Saulo na mutumishi wake walipofika kule Gibea, alipokelewa na kundi la manabii. Roho wa Mungu alimufikia kwa nguvu, na Saulo akaanza kutabiri pamoja na manabii hao.

11Watu waliomufahamu Saulo zamani, walipomwona anatabiri, wakaulizana: “Kitu gani kimemupata mwana wa Kisi? Hata Saulo ni mumoja wa manabii?”

12Mutu fulani, mukaaji wa pahali pale, akasema: “Baba yao ni nani?” Hivyo kukatokea mezali inayosema: “Hata Saulo ni mumoja wa manabii?”

13Saulo alipomaliza kutabiri, alikwenda kwenye nafasi ya kuabudia.

14Baba mudogo wa Saulo alipowaona Saulo na mutumishi, akawauliza: “Mulikuwa wapi?” Saulo akajibu: “Tulikwenda kuwatafuta punda, na tulipoona hawapatikani, tulikwenda kumwona Samweli.”

15Yule baba mudogo wa Saulo akamwambia: “Tafazali, uniambie kile Samweli alichokuambia.”

16Saulo akajibu: “Alituambia waziwazi kwamba punda wamepatikana.” Lakini Saulo hakumwelezea kwamba Samweli alimwambia kwamba atakuwa mufalme.

Saulo anatangazwa kuwa mufalme

17Samweli aliwaita watu wote wakusanyike mbele ya Yawe kule Misipa.

18Walipofika aliwaambia: “Yawe, Mungu wa Israeli, anasema hivi: Niliwatoa Waisraeli katika inchi ya Misri, nikawaokoa ninyi kutoka kwa Wamisri na falme zingine zilizowagandamiza.

19Lakini leo hii mumenikataa mimi Mungu wenu ambaye ninawaokoa kutoka hasara na huzuni zenu, nanyi mumesema: ‘Hapana! Utuwekee mufalme juu yetu.’ Sasa basi, mujikusanye wote mbele yangu mukiwa katika makabila yenu na kwa maelfu yenu.”

20Kisha Samweli akayapanga makabila yote ya Waisraeli, kabila la Benjamina likaangukiwa na kura.

21Akalileta mbele kabila la Benjamina, kulingana na ukoo zake, na ukoo wa Matiri ukachaguliwa kwa kura. Mwisho akauleta mbele ukoo wa Matiri, na Saulo mwana wa Kisi akachaguliwa kwa kura. Lakini walipomutafuta hakupatikana.

22Wakamwuliza Mungu tena: “Kuna mutu zaidi anayekuja?” Yawe akawajibu: “Anajificha kwenye mizigo.”

23Basi, walikwenda mbio, wakamutafuta Saulo na kumuleta. Saulo aliposimama kati ya watu alikuwa murefu kuliko watu wote, kuanzia kwenye mabega.

24Samweli akawaambia watu wote: “Huyu ndiye mutu aliyechaguliwa na Yawe kati ya watu wote; hakuna yeyote anayekuwa kama yeye.” Watu wote wakapiga kelele: “Mufalme aishi milele.”

25Kisha, Samweli aliwaelezea watu juu ya mapaswa na haki za mufalme, akaziandika katika kitabu ambacho alikiweka mbele ya Yawe. Kisha, Samweli aliwaaga watu wote, kila mutu aende kwake.

26Vilevile, Saulo pamoja na wapiganaji hodari ambao zamani Mungu aligusa mioyo yao, alikwenda kwake kule katika muji wa Gibea.

27Lakini watu wengine wasiofaa kitu, walisema: “Mutu huyu anaweza kutuokoa?” Walimuzarau Saulo na hawakumupa zawadi yoyote. Lakini yeye hakukasirika.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help