1“Mukienda kwa vita kupigana na waadui zenu, mukiona farasi, magari na jeshi kubwa zaidi kuliko lenu musiwaogope. Maana Yawe, Mungu wenu, aliyewatoa Misri, atakuwa nanyi.
2Mbele ya kuanza mapigano, kuhani atajitokeza mbele na kuwaambia watu:
3‘Watu wa Israeli musikilize! Leo munakaribia kupigana na waadui zenu. Musivunjike moyo, au kuogopa, au kutishwa, au kuwaogopa waadui;
4maana Yawe, Mungu wenu, ndiye atakayekwenda pamoja nanyi kupigana kwa ajili yenu mbele ya waadui zenu na kuwapa ushindi’.
5“Kisha wakubwa watawaambia watu: ‘Kuna mutu yeyote hapa aliyejenga nyumba mupya lakini hajaizindua? Arudie kwake, kusudi asikufie kwenye vita na mutu mwingine aizindue.
6Kuna mutu yeyote hapa aliyepanda mizabibu na ambaye hajafurahia matunda yake ya kwanza? Arudi kwake asikufie kwenye vita na mutu mwingine afurahie matunda yake.
7Kuna mwanaume yeyote hapa aliyechumbia na yuko karibu kuoa? Arudie kwake, kusudi asikufie kwenye vita, na mwanaume mwingine aoe muchumba wake.
8Kuna mutu aliyevunjika moyo? Arudie kwake, kusudi asiwavunje wenzake moyo kama vile yeye.’
9Wakubwa wakisha kusema na watu, basi majemadari watawaongoza watu.
10“Munapokaribia muji kwa kuushambulia, kwanza muwape wakaaji wake masharti ya amani.
11Wakaaji wa muji huo wakitaka amani na kujitoa kwenu, basi watu wote wanaokuwa humo watawatumikia na kufanya kazi za kulazimishwa.
12Lakini wakaaji wa muji huo wasipofanya amani nanyi, lakini wakipigana vita nanyi, basi, mutazunguka muji wao kwa vita,
13naye Yawe, Mungu wenu, akiutia katika mikono yenu, mutawaua kwa upanga wanaume wote.
14Lakini wanawake na watoto, ngombe, na vyote vinavyokuwa katika muji, vitu vyake vyote munaweza kuvibeba kwa ajili yenu wenyewe. Munaweza kufurahia vitu vya waadui zenu, ambavyo Yawe, Mungu wenu, amewapa.
15Ndivyo mutakavyoitendea miji yote ambayo iko mbali na inchi mutakayorizi.
16Lakini katika miji ya inchi ambayo Yawe, Mungu wenu, anawapa, musiache kitu chochote.
17Mutawaangamiza watu wote: Wahiti, Waamori, Wakanana, Waperizi, Wahivi na Wayebusi kama vile Yawe, Mungu wenu alivyoamuru,
18kusudi wasiwafundishe desturi zao za kuchukiza ambazo wanafanyia miungu yao, nanyi mutende zambi mbele ya Yawe, Mungu wenu.
19“Munapozunguka muji kwa muda murefu, mukipigana vita na kuuteka, musiharibu miti ya matunda kwa mashoka. Miti ni watu hata ishambuliwe nanyi? Munaweza kula matunda ya miti hiyo, lakini musiikate.
20Munaweza kukata tu miti mingine kwa kuitumia kwa kujenga ngazi za kupandia ndani ya muji munaoshambulia mpaka uanguke.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.