1-2Kwa mukubwa wa waimbaji: kwa vyombo vyenye nyuzi. Mashairi ya Daudi, yanayoelekea wakati mutu mumoja kutoka Zifu alipomwendea Saulo na kumujulisha kwamba Daudi amejificha kwao.
3Ee Mungu,
uniokoe kwa jina lako,
unitetee kwa nguvu zako.
4Ee Mungu, usikilize maombi yangu;
uyategee sikio maneno ya kinywa changu.
5Watu wenye kiburi wananishambulia,
watu wakali wanawinda maisha yangu,
watu ambao hawamujali Mungu.
6Ninajua Mungu ni musaada wangu,
Yawe anaimarisha maisha yangu.
7Yeye atawaazibu waadui zangu kwa uovu wao wenyewe;
kwa uaminifu wako, ee Mungu, uwaangamize.
8Nitakutolea sadaka kwa moyo wa furaha;
nitalisifu jina lako maana wewe ni muzuri.
9Umeniokoa katika taabu zangu zote,
nami nimewaona waadui zangu wameshindwa.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.