Amosi 1 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Nabii Amosi

1Haya ni maneno ya Amosi, mumoja wa wachungaji wa nyama wa muji wa Tekoa. Mungu alimufunulia Amosi mambo haya yote juu ya inchi ya Israeli miaka miwili mbele ya tetemeko la inchi, wakati Uzia alipokuwa mufalme wa Yuda, na Yeroboamu mwana wa Yoasi alipokuwa mufalme wa Israeli.

2Amosi alisema hivi:

Yawe ananguruma toka mulima Sayuni,

anavumisha sauti yake toka Yerusalema,

hata mashamba ya malisho ya wachungaji yanakauka,

majani ya mulima Karmeli yananyauka.

Hukumu ya Mungu kwa mataifa jirani ya IsraeliDamasiki

3Yawe anasema hivi:

Kwa sababu ya makosa matatu ya watu wa Damasiki, hata kwa mane,

sitageuza nia yangu.

Wamekatakata watu wa Gileadi wakitumia majembe ya mashini ya kulima.

4Basi, nitashusha moto juu ya nyumba ya mufalme Hazaeli,

na kuziteketeza kabisa nyumba nzuri za mufalme Beni-Hadadi.

5Nitavivunjavunja vifungio vya milango ya muji wa Damasiki,

na kuwaondoa wakaaji wa bonde la Aweni,

pamoja na mutawala wa Beti-Edeni.

Waaramu wanapelekwa katika uhamisho kule Kiri.

–Ni Yawe anayesema hivyo.

Wafilistini

6Yawe anasema hivi:

Kwa sababu ya makosa matatu ya watu wa Gaza, hata kwa mane,

sitageuza nia yangu.

Wamekamata watu wengi

na kuwapeleka kwa Waedomu.

7Basi, nitashusha moto juu ya kuta za muji wa Gaza,

na kuziteketeza kabisa nyumba zake nzuri.

8Nitaondoa wakaaji wa muji wa Asidodi,

pamoja na mutawala wa Asikeloni.

Nitanyoosha mukono wangu kwa kuazibu muji wa Ekuroni,

na Wafilistini wote waliobaki wataangamia.

Ni mimi Yawe ninayesema hivyo.

Tiro

9Yawe anasema hivi:

Kwa sababu ya makosa matatu ya watu wa Tiro, hata kwa mane,

sitageuza nia yangu.

Wamekamata watu wengi

na kuwapeleka mpaka Edomu.

Hawakutii mapatano ya urafiki waliokuwa wamefanya.

10Basi, nitashusha moto juu ya kuta za muji wa Tiro,

na kuziteketeza kabisa nyumba zake nzuri.

Edomu

11Yawe anasema hivi:

Kwa sababu ya makosa matatu ya watu wa Edomu, hata kwa mane,

sitageuza nia yangu.

Wamewawinda wandugu zao Waisraeli kwa mapanga,

wakaitupilia mbali huruma yao yote ya kindugu.

Hasira yao haikuwa na mwisho,

waliiacha iwake siku zote.

12Basi, nitashusha moto juu ya muji wa Temani,

na kuziteketeza kabisa nyumba nzuri za Bosira.

Amoni

13Yawe anasema hivi:

Kwa sababu ya makosa matatu ya watu wa Amoni, hata kwa mane,

sitageuza nia yangu.

Katika vita yao kwa kupanua inchi,

walipasua tumbo za wanawake wenye mimba katika inchi ya Gileadi.

14Basi, nitashusha moto juu ya kuta za muji wa Raba,

na kuziteketeza kabisa nyumba zake nzuri.

Siku hiyo ya vita kutakuwa makelele mengi,

nayo mapambano yatakuwa makali kama zoruba.

15Mufalme wao na wakubwa wake,

wote watakwenda kukaa katika uhamisho.

–Ni Yawe anayesema hivyo.

Moabu
Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help