1Zaburi ya shukrani. Mumushangilie Yawe, enyi inchi zote!
2Mumwabudu Yawe kwa furaha,
mukuje mbele yake mukiimba kwa shangwe!
3Mujue kwamba Yawe ndiye Mungu.
Yeye ndiye aliyetuumba, sisi ni mali yake;
sisi ni watu wake na kondoo wake anaowachunga.
4Muingie ndani ya hekalu lake kwa shukrani,
muingie katika kiwanja chake kwa kumusifu.
Mumushukuru na kulisifu jina lake.
5Yawe ni muzuri!
Wema wake unadumu milele,
na uaminifu wake kwa vizazi vyote.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.