1Zaidi ya hayo yote, utatengeneza hema takatifu kwa mapazia kumi ya kitani safi iliyosokotwa, na kwa sufu ya rangi ya samawi, zambarau na nyekundu. Mapazia hayo utayapamba kwa makerubi waliochorwa.
2Kila pazia litakuwa na urefu wa metre kumi na mbili na upana wa metre mbili. Mapazia hayo yakuwe ya kipimo kimoja.
3Utaunganisha mapazia matano yakuwe kipande kimoja na mapazia mengine matano yakuwe kipande cha pili.
4Utashonea kamba za rangi ya samawi kwenye upindo wa pazia la mwisho la kipande cha kwanza. Vilevile utashonea kamba kwa mwisho wa pindo la inje la kipande kingine cha pazia.
5Utatia kamba makumi tano katika pazia moja na kamba zingine makuni tano kwenye utepe wa pazia la pili, kamba zote zielekeane.
6Kisha utatengeneza vifungio makumi tano vya zahabu kwa kuunganishia vile vipande viwili vya mapazia, hivyo hema litakuwa kitu kimoja.
7Vilevile utatengeneza kifuniko cha hema kwa mapazia kumi na moja ya manyoya ya mbuzi.
8Kila pazia litakuwa na urefu wa metre kumi na tatu na upana wa metre mbili. Mapazia yote yale kumi na moja yatakuwa na kipimo kilekile.
9Utaunga mapazia matano pamoja na mapazia sita pamoja. Pazia la sita utalikunja mara mbili mbele ya hema.
10Kisha utafanya kamba makumi tano kwenye upindo wa pazia la mwisho la kipande cha kwanza na kamba makumi tano kwenye upindo wa pazia la mwisho la kipande cha pili.
11Utatengeneza vifungio makumi tano vya shaba na kuviingiza katika zile kamba makuni tano kwa kuunganishia vile vipande viwili vya mapazia na hivyo kufanya pazia moja la hema.
12Ile nusu ya pazia iliyobaki utaitundika upande wa nyuma wa hema.
13Nusu metre ya urefu wa mapazia iliyokuwa ya zaidi utaikunja ininginie pande zote kwenye mbavu ya hema kwa kulifunika.
14Utatengeneza vilevile kifuniko kingine cha hema kilichofanywa kwa ngozi laini ya kondoo dume na ngozi laini ya mbuzi.
15Utatengeneza mbao za mujohoro za kusimama wima kwa ajili ya hema.
16Kila ubao utakuwa na urefu wa metre ine na upana wa sentimetre makumi sita na sita.
17Kila ubao utakuwa na ndimi mbili za kuunganishia. Utazifanyia mbao zote ndimi mbili.
18Basi, utatengeneza zile mbao za hema hivi: mbao makumi mbili kwa ajili ya upande wa kusini,
19na vikalio makumi ine vya feza chini ya zile mbao makumi mbili, vikalio viwili chini kwa kila ubao kwa kushikilia zile ndimi zake mbili na vikalio viwili vikuwe chini ya ubao mwingine kwa kushikilia zile ndimi zake mbili.
20Upande wa kaskazini wa hema, utatengeneza mbao makumi mbili,
21na vikalio vyake makumi ine vya feza, vikalio viwili chini ya kila ubao.
22Kwa upande wa nyuma, unaokuwa kwa upande wa magaribi wa hema, utatengeneza mbao sita.
23Utatengeneza vilevile mbao mbili kwa ajili ya pembe za hema upande wake wa nyuma.
24Mbao zile za pembeni ziachane chini lakini zishikamanishwe kwa juu kwenye pete ya kwanza. Mbao zote za pembeni zifanywe vile vile kusudi zifanye pembe mbili.
25Hivyo kutakuwa mbao nane pamoja na vikalio vyake kumi na sita vya feza: vikalio viwili chini ya kila mbao na vikalio viwili chini ya ubao mwingine.
26Utatengeneza miti ya mujohoro; miti tano kwa ajili ya mbao za upande mumoja wa hema,
27na miti tano kwa ajili ya upande wa pili wa hema, na miti tano kwa ajili ya mbao za upande wa nyuma wa hema, kwa upande wa magaribi.
28Muti wa katikati uliofika nusu ya jengo la hema utapenya katikati toka mwisho huu mpaka mwisho mwingine wa hema.
29Mbao zote utazipakaa zahabu na kuzifanyia pete za zahabu zitakazoshikilia ile miti, ambazo vilevile utazipakaa zahabu.
30Hivyo utalitengeneza hema hilo kulingana na mufano niliokuonyesha juu ya mulima.
31Utatengeneza pazia la nyuzi za rangi ya samawi, zambarau na nyekundu na kitani safi iliyosokotwa. Juu ya pazia lile utachora kwa ufundi sanamu za makerubi.
32Utalitundika pazia kwenye nguzo ine za mujohoro zilizopakwa zahabu, zenye vifungio vya zahabu na vikalio vine vya feza.
33Utatundika pazia lile kwenye vifungio, kisha ulete lile Sanduku la Agano mule ndani, nyuma ya pazia lile. Pazia lile litatenga Pahali Patakatifu na Pahali Patakatifu Sana. Ang. Ebr 6.19; 9.3-5
34Ndani ya Pahali Patakatifu utaweka kile kiti cha rehema juu ya Sanduku la Agano.
35Ile meza ya mujohoro utaiweka upande wa inje wa pazia lile, na kile kinara cha taa utakiweka upande wa kusini wa hema, kikielekeana na meza. Meza ile itakuwa upande wa kaskazini.
36Kwa ajili ya mulango wa hema utatengeneza pazia zito kwa sufu ya rangi ya samawi, zambarau na nyekundu, na kitani safi iliyosokotwa, na kuchorwa vizuri.
37Vilevile utatengeneza nguzo tano za mujohoro na kuzipakaa zahabu. Nguzo hizo zitakuwa na vifungio vya zahabu, na kila moja itakuwa na tako la shaba.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.