Kutoka 34 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Vibao vipya vya agano(Kumb 10.1-5)

1Yawe akamwambia Musa: Chonga vibao viwili vya mawe kama vile vya kwanza, nami nitaandika maneno yale yaliyokuwa katika vile vibao vya kwanza ulivyovunja.

2Ukuwe tayari kesho asubui, ukuje kukutana nami juu ya mulima Sinai.

3Mutu yeyote asikuje pamoja nawe, wala asionekane popote kwenye mulima, wala kondoo au ngombe wasikulishwe karibu yake.

4Basi, Musa akachonga vibao viwili vya mawe kama vile vya kwanza. Akaondoka asubui mapema, akapanda juu ya mulima Sinai, kama vile Yawe alivyomwamuru, akiwa na vile vibao viwili vya mawe katika mikono yake.

5Yawe akashuka katika wingu, akasimama pamoja na Musa, akataja jina lake: Yawe.

6Kisha Yawe akapita mbele ya Musa akitangaza tena:

Yawe, Yawe,

ni Mungu mwenye rehema na huruma,

si mwepesi wa hasira,

ni mwingi wa wema na uaminifu.

7Anawatendea mema maelfu,

anawasamehe uovu, makosa na zambi.

Lakini hataacha kumwazibu mwenye kosa.

Anawalipiza watoto na wajukuu

uovu wa baba na babu zao,

hata kizazi cha tatu na cha ine.

8Musa akainama uso mpaka chini haraka, akamwabudu Mungu.

9Kisha akasema: Ee Bwana wangu, kama nimepata kukubaliwa mbele yako, ninakuomba uende pamoja nasi. Watu hawa ni wenye vichwa vigumu, lakini utusamehe uovu wetu na zambi yetu, utupokee kama watu wako mwenyewe.

Agano linafanywa upya(Kut 23.14-19; Kumb 7.1-5; 16.1-17)

10Yawe akamwambia Musa: Sasa ninafanya agano na watu wako. Nitatenda maajabu mbele yao ambayo hayajapata kutendwa katika dunia yote, wala katika taifa lolote. Na watu wote munaoishi kati yao wataona matendo yangu makubwa. Maana nitafanya jambo la ajabu kwa ajili yako.

11Mushike amri ninazowapa leo. Nitawafukuza mbele yenu Waamori, Wakanana, Wahiti, Waperizi, Wahivi na Wayebusi.

12Mufanye angalisho musifanye agano na wakaaji wa inchi munayoiendea, maana hiyo itakuwa mutego kati yenu.

13Lakini mutabomoa mazabahu zao na kuvunja nguzo zao za ibada na sanamu zao za Ashera.

14Musiabudu mungu yeyote mwingine, maana mimi Yawe ninajulikana kwa jina: Mwenye Wivu. Mimi ni Mungu mwenye wivu.

15Musifanye mapatano yoyote na wakaaji wa inchi hiyo, maana watakapoabudu miungu yao ya uongo na kuitambikia, watawaalika, nanyi mutashawishiwa kula vyakula wanavyotambikia miungu yao.

16Vijana wenu wakioa wabinti zao, na hao wabinti wanaoabudu miungu yao, watawashawishi vijana wenu kufuata miungu yao.

17Musijifanyie miungu ya uongo ya chuma.

18Mutashika sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu. Kwa muda wa siku saba mutakula mikate isiyotiwa chachu wakati uliopangwa katika mwezi wa Abibu, kama vile nilivyowaamuru, kwa sababu katika mwezi huo wa Abibu mulitoka Misri.

19Kila muzaliwa wa kwanza mwanaume ni wangu, pamoja na wazaliwa wa kwanza dume wa nyama wako wote, wa ngombe na wa kondoo. kwa mwanzo wa wakati wa mavuno ya ngano na kufanya sikukuu ya kukusanya mavuno kwa mwisho wa mwaka.

23Mara tatu kwa mwaka wanaume wote watakusanyika mbele ya Bwana wenu, Yawe, Mungu wa Israeli.

24Nitafukuza mataifa mengine mbele yenu na kupanua mipaka yenu. Hakuna mutu yeyote atakayetamani inchi yenu wakati munapokusanyika kwa kuniabudu, mimi Yawe, Mungu wenu, mara tatu kila mwaka.

25Musinitolee damu ya sadaka yangu pamoja na chachu, wala sadaka ya sikukuu ya Pasaka isiachwe mpaka asubui.

26Mazao ya kwanza ya shamba yako utayaleta katika nyumba yangu mimi Yawe, Mungu wako.

Usipike mwana-kondoo au mwana-mbuzi katika maziwa ya mama yake.

27Yawe akamwambia Musa: Andika maneno haya, maana kulingana na maneno haya, ninafanya agano nawe na watu wa Israeli.

28Musa alikaa kule kwenye mulima pamoja na Yawe siku makumi ine, muchana na usiku. Hakukula chakula wala kunywa maji. Aliandika maneno yote ya agano na zile amri kumi.

Musa anashuka kutoka kwenye mulima Sinai

29Musa alipokuwa anashuka toka kwenye mulima Sinai akiwa na vile vibao viwili vyenye maneno ya agano katika mikono yake, hakujua kwamba uso wake ulikuwa unangaa kwa sababu alikuwa ameongea na Yawe. Ang. 2 Kor 3.7-16

30Haruni na watu Waisraeli wote walipomwona wakaogopa kumukaribia, maana uso wake ulikuwa unangaa.

31Lakini Musa alimwita Haruni na viongozi wote wa Waisraeli waende karibu naye, kisha akazungumuza nao.

32Kisha Waisraeli wote wakakuja karibu naye, naye akawapa amri zote ambazo Yawe alimupa kule juu ya mulima Sinai.

33Musa alipomaliza kuzungumuza na watu akaufunika uso wake kwa kitambaa.

34Lakini ikakuwa kwamba kila mara Musa alipokwenda kuongea na Yawe katika hema la mukutano, aliondoa kile kitambaa mpaka alipotoka inje. Na alipotoka inje aliwaambia Waisraeli mambo yote aliyoamuriwa,

35nao Waisraeli waliona uso wake unangaa. Halafu Musa alifunika tena uso wake kwa kitambaa mpaka alipokwenda kuongea na Yawe.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help