1 Wafalme 18 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Elia mbele ya mufalme na manabii wa Bali

1Nyuma ya siku nyingi, katika mwaka wa tatu wa ukosefu wa mvua, neno la Yawe lilimufikia Elia kusema hivi: “Kwenda ujionyeshe kwa mufalme Ahabu, halafu nitanyesha mvua katika inchi.”

2Basi, Elia akaenda kujionyesha kwa Ahabu.

Wakati huo, njaa ilikuwa kali sana kule Samaria.

3Basi, Ahabu akamwita Obadia musimamizi wa nyumba ya kifalme. Obadia alikuwa mutu anayemwogopa Yawe sana,

4na wakati Yezebeli alipowaua manabii wa Yawe, Obadia aliwachukua manabii mia moja, akawaficha makumi tano tano ndani ya pango, akakuwa anawapelekea chakula na maji.

5Ahabu akamwambia Obadia: “Labda tutapata majani na pale tutaokoa farasi na nyumbu wetu wamoja.”

6Basi, wakagawanyana inchi kusudi wapate kuichunguza yote. Ahabu akaenda upande mumoja na Obadia upande mwingine.

7Obadia alipokuwa katika njia, alikutana na Elia; naye Obadia alipomutambua Elia, aliinama chini na kusema: “Hakika, ni wewe bwana wangu Elia?”

8Elia akamwambia: “Ndiyo! Ni mimi Elia. Kwenda umwambie bwana wako kwamba niko hapa.”

9Obadia akasema: “Nimefanya kosa gani hata utake kunitia katika hatari kusudi niuawe na mufalme Ahabu?

10Ninakuapia kwa jina la Yawe, Mungu wako, Mwenye Uzima, kwamba mufalme amekuwa akikutafuta katika dunia yote. Na mufalme yeyote akisema kwamba haujaonekana kule, Ahabu alimutaka huyo mufalme aape na watu wake kwamba kweli hauko.

11Na sasa, unataka niende kumwambia kwamba wewe uko hapa!

12Ninaogopa kwamba mara tu nitakapoondoka, Roho wa Yawe atakunyanyua na kukupeleka pahali nisipopajua! Nikienda kumwambia Ahabu kwamba uko hapa, naye akikutafuta na asikupate, ataniua mimi, ingawa mimi mutumishi wako ninamwogopa Yawe tangu ujana wangu.

13Hauna habari kwamba Yezebeli alipokuwa akiwaua manabii wa Yawe, mimi niliwatwaa manabii mia moja nikawaficha makumi tano tano katika pango, nikakuwa ninawapatia chakula na maji?

14Sasa unaniambia niende kumwambia bwana wangu kwamba wewe Elia uko hapa! Ahabu ataniua.”

15Elia akamwambia: “Kama vile Yawe wa majeshi anavyoishi, yule ambaye ninamutumikia: leo hii nitajitokeza mbele ya mufalme.”

16Basi, Obadia akaenda kwa mufalme Ahabu, akamupa habari hizo. Naye Ahabu akaenda kukutana na Elia.

17Ahabu alipomwona Elia, alisema: “Hakika ni wewe unayetaabisha Waisraeli?”

18Elia akamujibu: “Mwenye kutaabisha Waisraeli si mimi, lakini ni wewe na jamaa ya baba yako. Ninyi mumepita pembeni ya amri za Yawe na kuabudu Bali.

19Sasa, uwakusanye watu wote wa Israeli mbele yangu kule kwenye mulima Karmeli. Vilevile, uwakusanye wale manabii mia ine na makumi tano wa Bali, na manabii mia ine wa Ashera ambao wanakulishwa na malkia Yezebeli.”

20Basi, Ahabu akawaita watu wote wa Israeli, akawakusanya na manabii wote kule kwenye mulima Karmeli.

21Kisha, Elia akawakaribia watu hao, akawaambia: “Mutaendelea kusitasita ndani ya mioyo mpaka wakati gani? Ikiwa Yawe ni Mungu, mumufuate; lakini ikiwa Bali ni Mungu, basi, mumufuate.”

Lakini watu hawakumujibu neno lolote.

22Halafu, Elia akawaambia: “Mimi peke yangu tu ndiye nabii wa Yawe niliyebaki, lakini manabii wa Bali wapo mia ine na makumi tano.

23Basi! Mulete ngombe dume wawili. Manabii wa Bali wajichagulie ngombe dume mumoja, wamuchinje, wamukate vipandevipande na kumuweka juu ya kuni, bila kuwasha moto. Nami vilevile nitamutwaa yule ngombe dume mwingine, nitamuchinja na kumuweka juu ya kuni bila kuwasha moto.

24Kisha, wao watamwomba mungu wao, nami nitamwomba Yawe. Mungu atakayejibu kwa kuleta moto, yule ndiye Mungu wa kweli.”

Na pale watu wote wakasema: “Sawa!”

25Kisha, Elia akawaambia manabii wa Bali: “Ninyi ni wengi. Basi, muanze. Mujichagulie, mutayarishe ngombe dume, mumutayarishe na kumwomba mungu wenu, lakini musiwashe moto.”

26Hao manabii wakamutwaa ngombe dume wao waliyepewa, wakamutayarisha, kisha wakaanza kumulilia Bali kutokea asubui mpaka saa sita za muchana, wakirukaruka pembeni ya mazabahu waliyotengeneza wakisema: “Ee Bali, utusikilize!”

Lakini hakukutokea sauti yoyote, wala hakuna aliyewajibu.

27Ilipofika saa sita muchana, Elia akaanza kuwachekelea akisema: “Muombe kwa sauti kubwa zaidi! Yeye ni mungu, labda iko na kazi nyingi au ametoka na kusafiri! Labda analala, munapaswa kumwamusha!”

28Manabii hao wakapiga kelele zaidi, wakajikatakata kwa visu na wembe, kufuatana na desturi yao, hata damu ikawatiririka.

29Wakaendelea kupiga makelele na kufanya kama vile wenda-wazimu mpaka nyuma ya saa sita wakati wa kutoa sadaka. Lakini hakuna aliyewajibu wala kuwajali.

30Basi, Elia akawaambia watu: “Musogee karibu nami.”

Wao wakamukaribia. Kisha Elia akaijenga upya mazabahu ya Yawe iliyokuwa imebomolewa.

31Alitwaa mawe kumi na mawili, hesabu ya makabila kumi na mawili yaliyopewa majina ya wana wa Yakobo ambaye neno la Yawe lilimufikia kusema hivi: “Jina lako litakuwa Israeli.”

32Kwa mawe hayo, Elia alimujengea Yawe mazabahu. Akachimba mufereji pembenipembeni ya mazabahu hiyo, mufereji ambao unaweza kujazwa na maji yapata litre kumi na ine.

33Kisha akapanga kuni vizuri, akakata vipandevipande ile ngombe dume, akaviweka juu ya kuni.

Kisha akawaambia watu: “Mujaze mitungi mine maji muimwangie juu ya sadaka hii ya kuteketezwa pamoja na kuni.” Wakafanya hivyo.

34Kisha akawaambia: “Mufanye hivyo tena.” Nao wakafanya hivyo kwa mara ya pili. Naye akawaambia: “Mufanye hivyo tena kwa mara ya tatu.” Nao wakafanya hivyo.

35Maji yakatiririka chini pande zote za mazabahu, hata yakajaa ndani ya mufereji.

36Kwa wakati wa kutoa sadaka ya magaribi, nabii Elia aliikaribia mazabahu, akaomba: “Ee Yawe, Mungu wa Abrahamu, Isaka na Yakobo, uwaonyeshe watu leo hii kwamba wewe ndiwe Mungu wa Israeli, na kwamba mimi ni mutumishi wako na nimefanya mambo haya kwa amri yako.

37Unijibu, ee Yawe, unijibu kusudi watu hawa wajue kwamba wewe Yawe ndiwe Mungu, na kwamba umeigeuza mioyo yao wakurudilie.”

38Mara moja, Yawe akashusha moto, ukaiteketeza sadaka ile ya kuteketezwa, kuni, mawe na mavumbi, na kuyakausha maji yote katika mufereji.

39Watu walipoona hivyo, walianguka uso mpaka chini na kusema: “Yawe ndiye Mungu! Yawe ndiye Mungu!”

40Halafu Elia akawaambia: “Muwakamate manabii wote wa Bali. Musimwache hata mumoja wao atoroke!” Basi, watu wakawakamata wote, naye Elia akawapeleka kwenye muto Kisoni, akawauia kule.

Mwisho wa ukosefu wa mvua

41Nyuma ya hayo, Elia akamwambia mufalme Ahabu: “Kwenda kula na kunywa. Ninasikia kishindo cha mvua.”

42Basi, Ahabu akaenda zake kula na kunywa.

Naye Elia akapanda juu ya kilele cha mulima Karmeli, na kule akainama uso mpaka chini na kuuweka uso wake katikati ya magoti yake.

43Kisha akamwambia mutumishi wake: “Sasa, kwenda uangalie kwa upande wa bahari.”

Mutumishi akaenda, akaangalia, kisha akarudia akasema: “Hakuna kitu.”

Elia akamwambia: “Kwenda tena mara saba.”

44Kwa mara ya saba, yule mutumishi akarudia, akasema: “Ninaona wingu dogo kama mukono wa mutu linatoka katika bahari.”

Elia akamwambia: “Kwenda umwambie mufalme Ahabu atayarishe gari lake la vita, ateremuke, asipate kuzuiliwa na mvua.”

45Nyuma ya wakati kidogo mbingu zikatanda mawingu mazito, upepo ukavuma, kukanyesha mvua kubwa. Ahabu naye akapanda ndani ya gari lake la vita, akarudia Yezereheli.

46Nguvu ya Yawe ikamufikia Elia, naye akajitayarisha kusafiri, akakimbia na kumutangulia Ahabu kuingia ndani ya muji Yezereheli.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help