Waebrania 1 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Mungu anasema na watu kwa njia ya Mwana wake

1Zamani Mungu alisema na babu zetu kwa njia ya manabii, mara nyingi na kwa namna nyingi.

2Lakini kwa siku hizi za mwisho amesema nasi kwa njia ya Mwana wake. Mungu alimuweka kuwa murizi wa vitu vyote, na ambaye kwa njia yake aliumba ulimwengu wote.

3Yeye ni kitambulisho cha mwangaza wa utukufu wa Mungu, kwa maana yeye ni mufano kamili pahali ya Mungu mwenyewe, na kwa uwezo wa neno lake analinda vitu vyote. Naye alipokwisha kuwatakasa watu toka katika zambi zao, aliikaa na mamlaka katika mbingu kwa kuume kwa Mungu Mwenye Uwezo wote.

Kristo ni mukubwa kuliko wamalaika

4Mwana amepata kuwa mukubwa kupita wamalaika kufuatana na lile jina alilopewa na Mungu, linalokuwa tukufu kuliko jina lao.

5Kwa maana Mungu hakumwambia hata mara moja mumoja wa wamalaika wake hivi:

“Wewe ni mwana wangu,

mimi leo nimekuwa baba yako.”

Wala hakusema maneno haya juu ya malaika yeyote:

“Mimi nitakuwa Baba yake,

naye atakuwa Mwana wangu.”

6Na tena wakati Mungu alipomutuma muzaliwa wake wa kwanza katika dunia, alisema:

“Wamalaika wote wa Mungu wanapaswa kumwabudu.”

7Lakini juu ya wamalaika, Mungu alisema:

“Mungu anawafanya wamalaika wake kuwa kama upepo.

Anawafanya hao watumishi wake kuwa kama ndimi za moto.”

8Lakini juu ya Mwana, Mungu alisema:

“Kiti chako cha kifalme, Ee Mungu,

kitadumu hata milele.

Unatawala ufalme wako kwa haki.

9Unapenda haki na kuchukia uovu.

Ni kwa hiyo Mungu, Mungu wako,

amekusimika,

akikupakaa mafuta,

akikupatia heshima

na kukuinua juu kuliko wenzako wote.”

10Vilevile Mungu alisema:

“Wewe Bwana, kwa mwanzo uliumba dunia,

mbingu ni kazi ya mikono yako.

11Vitatoweka lakini wewe utabaki.

Vitachakaa kama nguo.

12Utavikunjakunja kama kanzu,

navyo vitabadilishwa kama nguo.

Lakini wewe utabaki sawasawa, na maisha yako hayatakuwa na mwisho.”

13Mungu hakumwambia hata mara moja mumoja wa wamalaika wake hivi:

“Ikaa na mamlaka kwa kuume kwangu,

mpaka nitakapowaweka waadui zako chini ya miguu yako.”

14Malaika ni nini, basi? Wao wote ni roho wanaomutumikia Mungu na wanaotumwa naye kwa ajili ya faida ya wale wanaopaswa kuokolewa.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help