1Ilikuwa nyuma ya Nebukadneza mufalme wa Babeli kuwahamisha Yekonia mufalme wa Yuda mwana wa Yoyakimu, pamoja na wakubwa wa inchi ya Yuda na wafundi bora na wafuaji wa vyuma kutoka Yerusalema na kuwapeleka Babeli. Yawe akanionyesha vikapu viwili vya matunda ya tini vimewekwa mbele ya hekalu la Yawe.
2Ndani ya kikapu cha kwanza kulikuwa tini nzuri sana, kama vile tini za mavuno ya kwanzakwanza. Lakini ndani ya kikapu cha pili kulikuwa tini mbaya sana, mbaya hata hazifai kukuliwa.
3Basi, Yawe akaniuliza: Yeremia! Unaona nini? Mimi nikamujibu: Ninaona tini. Zile nzuri ni nzuri sana, na zile mbaya ni mbaya sana hata hazifai kukuliwa.
4Halafu neno la Yawe lilinifikia kusema hivi:
5Yawe, Mungu wa Israeli, anasema hivi: Kama tini hizi zinavyokuwa nzuri, ndivyo nitakavyowaona kuwa wema watu wa Yuda ambao niliowaondoa toka nafasi hii na kuwapeleka katika uhamisho katika inchi ya Wababeli.
6Nitawalinda siku zote na kuwarudisha katika inchi hii. Nitawajenga, wala sitawabomoa; nitawapanda, wala sitawaongoa.
7Nitawapa moyo wa kujua kwamba mimi ndimi Yawe. Watakuwa watu wangu, nami nitakuwa Mungu wao; maana watanirudilia kwa moyo wao wote.
8Yawe anasema hivi: Na kama vile wanavyozitendea zile tini mbaya, tini zinazokuwa mbaya hata hazifai kukuliwa, ndivyo nitakavyowatendea mufalme Zedekia wa Yuda, wakubwa wa serikali yake pamoja na watu wengine wote wa Yerusalema waliobaki katika inchi hii, na vilevile wale ambao walihamia katika inchi ya Misri.
9Nitawafanya kuwa kitu cha kuchukiza mbele ya falme zote za dunia. Watakuwa kitu cha zihaka, kitu cha kuzomewa, kuchekelewa na kulaaniwa kila fasi nitakapowasambaza.
10Na zaidi ya ile nitawaletea vita, njaa na magonjwa makali mpaka waangamizwe kabisa kutoka katika inchi niliyowapa wao na babu zao.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.