1Nyuma ya mambo hayo nilipata maono mengine. Niliona mulango mumoja umefunguliwa wazi mbinguni.
Halafu ile sauti niliyosikia mara ya kwanza, iliyolia kama baragumu, ikaniambia: “Panda huku, nami nitakuonyesha mambo yanayopaswa kutokea nyuma ya hayo ya mbele.”
2Na mara moja nikashikwa na Roho wa Mungu. Nikaona kiti cha kifalme kimewekwa kule mbinguni na mutu mumoja alikuwa akiikaa juu ya kiti kile.
3Mutu yule aliangaa kama mawe ya bei kali ya yaspi na sardio. Kiti kile cha kifalme kilikuwa kimezungukwa na upindi wa mvua uliongaa kama jiwe la zumaridi.
4Na kiti kile kilikuwa kimezungukwa na viti vingine makumi mbili na vine vya kifalme na juu ya viti vile kulikuwa kumeikaa wazee makumi mbili na wane. Wale wazee walikuwa wamevaa nguo nyeupe na juu ya kichwa chao kulikuwa taji za zahabu.
5Umeme ulipiga tokea katika kiti kile, na makelele na ngurumo ya radi vilisikilika. Mbele ya kiti kile kulikuwa kukiwaka mienge saba, na hizo ndizo zile roho saba za Mungu.
6Tena mbele ya kiti kile kulionekana kama bahari ya kioo, kulingaa sana kama kilauri.
Kile kiti cha kifalme kilikuwa kimezungukwa pande zote na viumbe vine vya ajabu, vyenye kujaa macho mbele na nyuma.
7Kiumbe cha kwanza kilifanana na simba, kiumbe cha pili kilifanana na mwana-ngombe na kiumbe cha tatu kilifanana na mutu na kiumbe cha ine kilifanana na tai anayeruka.
8Na kila kimoja cha viumbe vya ajabu kilikuwa na mabawa sita yenye kujaa macho ndani na inje. Navyo viliimba muchana na usiku bila kuchoka, vikisema:
“Mutakatifu, mutakatifu, mutakatifu ni Bwana wetu, Mungu Mwenye Uwezo,
aliyekuwa, anayekuwa na anayekuja.”
9Vile viumbe vine vya ajabu viliimba kwa kumutukuza, kumuheshimia na kumushukuru yule aliyeikaa juu ya kiti cha kifalme, yule anayeishi kwa milele na milele. Kila mara vilipofanya vile,
10wale wazee makumi mbili na wane waliinama uso mpaka chini mbele ya yule anayeikaa juu ya kiti cha kifalme, wakimwabudu huyo anayeishi kwa milele na milele. Nao walikuwa wakikuja kuweka taji zao mbele ya kiti chake, na kusema:
11“Bwana wetu na Mungu wetu, wewe unastahili utukufu, heshima na uwezo,
kwa maana wewe ndiwe uliyeumba vitu vyote;
vile vimeumbwa na kupata kuwa kutokana na mapenzi yako.”
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.