Danieli 10 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Maono ya Danieli kando ya muto Tigre

1Katika mwaka wa tatu wa utawala wa mufalme Kiro wa Persia, Danieli, aliyeitwa vilevile Beltesaza, alipewa ufunuo. Ufunuo huo ulikuwa wa kweli, lakini ulikuwa mugumu sana. Hata hivyo alielewa ufunuo huo maana alifahamu maono vilevile.

2Wakati huo, mimi Danieli, nilikuwa nikiomboleza kwa muda wa majuma matatu.

3Sikukula chakula kizuri, sikugusa nyama wala divai, na sikujipakaa mafuta kwa muda wa majuma hayo yote matatu.

4Siku ya makumi mbili na ine ya mwezi wa kwanza, nilikuwa nimesimama kando ya muto Tigre.

5Nikainua macho, nikamwona mutu anayevaa nguo za kitani naye alikuwa amejifunga mukaba wa zahabu safi kutoka Ufasi. Ang. Ufu 1.13-15; 2.18; 19.12

6Mwili wake ulingaa kama zabarajadi safi. Uso wake ulifanana na umeme, na macho yake yaliwaka kama ndimi za moto. Miguu na mikono yake ilingaa kama shaba iliyosafishwa sana. Sauti yake ilivuma kama sauti ya kundi kubwa la watu.

7Mimi Danieli peke yangu niliona maono hayo. Wale watu waliokuwa pamoja nami hawakuyaona, lakini walishikwa na hofu sana, wakakimbia, wakajificha.

8Hivyo, niliachwa peke yangu nikiangalia hayo maono ya kushangaza. Nguvu zikaniishia, na uso wangu ukabadilika rangi, nikabaki bila nguvu.

9Nilipoisikia sauti yake, nilianguka uso mpaka chini, nikashikwa na usingizi muzito.

10Hapo, mukono ukanigusa, ukanisimamisha, na kuimarisha miguu na mikono yangu.

11Akaniambia: Danieli, wewe unayependwa sana, simama sawa usikilize kwa uangalifu maneno nitakayosema, maana nimetumwa kwako. Alipokuwa akiniambia maneno haya, mimi nilisimama nikitetemeka.

12Kwa hiyo yeye akaniambia: Danieli, usiogope. Mungu alisikia maombi yako tangu siku ile ya kwanza ulipoamua kujinyenyekeza mbele yake kusudi upate ufahamu. Mimi nimekuja kwa ajili ya maombi yako hayo.

13Mukubwa wa ufalme wa Persia alinipinga kwa muda wa siku makumi mbili na moja. Lakini Mikaeli, mumoja kati ya wakubwa, akakuja kunisaidia, kwa hiyo nikamwacha kule pamoja na mukubwa wa ufalme wa Persia, Ang. Ufu 12.7

14nami nimekuja kukusaidia upate kuyafahamu mambo yatakayowapata watu wako wakati unaokuja, maana maono uliyoona yanaelekea wakati unaokuja.

15Alipokuwa ananiambia maneno hayo, niliangalia chini bila kuweza kusema.

16Kisha, kiumbe kimoja chenye umbo la mutu, kiliigusa midomo yangu, nami nilifungua midomo yangu na kumwambia huyo aliyesimama karibu nami: Ee bwana, maono haya yameniletea maumivu makali hata nimeishiwa nguvu.

17Mimi ni kama mutumwa mbele ya bwana wake. Ninaweza namna gani kusema nawe? Sina nguvu na pumzi imeniishia!

18Yule aliyeonekana kama mwanadamu akanigusa kwa mara ingine, akanitia nguvu.

19Akaniambia: Usiogope wewe unayependwa sana, uko salama. Ukuwe imara na hodari. Aliposema nami, nilipata nguvu, nikamwambia: Bwana, umekwisha kuniimarisha; sema kile ulichotaka kusema.

20Naye akaniambia: Unajua kwa nini nimekuja kwako? Sasa ninapaswa kurudi kwenda kupigana na malaika mulinzi wa Persia. Halafu, nitakapokuwa nimemushinda, malaika mulinzi wa mufalme wa Ugriki atatokea.

21Lakini nitakujulisha yale yaliyoandikwa katika kitabu cha ukweli. Sina mwingine wa kunisaidia kwa kuwashinda hawa isipokuwa Mikaeli, malaika mulinzi wenu.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help