1Kulikuwa mutu mumoja katika muji wa Rama katika inchi ya milima ya Efuraimu jina lake Elekana wa kabila la Efuraimu. Yeye alikuwa mwana wa Yerohamu, na mujukuu wa Elihu mwana wa Tohu mwana wa Zufu.
2Elekana alikuwa na wake wawili, mumoja aliitwa Hana na wa pili Penina. Penina alikuwa na watoto, lakini Hana hakukuwa na watoto.
3Kila mwaka Elekana alisafiri kutoka Rama kwenda kuabudu na kumutolea Yawe wa majeshi sadaka kule Shilo. Kule, wana wawili wa Eli, Hofuni na Finehasi, walikuwa makuhani wa Yawe.
4Kila wakati Elekana alipotoa sadaka alimupa muke wake Penina fungu moja la nyama ya sadaka na fungu mojamoja kwa watoto wake wa kiume na wa kike.
5Elekana alimupa Hana fungu kubwa la nyama ya sadaka kwa sababu alimupenda sana ingawa Yawe hakumujalia watoto.
6Penina alikuwa akimuchokoza sana Hana kusudi amukasirikishe kwa sababu Yawe hakumujalia Hana watoto.
7Mambo hayo yaliendelea kila mwaka. Kila mara Hana alipokwenda kwenye nyumba ya Yawe, Penina alimukasirikisha Hana hata Hana akalia na kukataa kula chochote.
8Mume wake Elekana alimwuliza: “Kwa nini unalia? Kwa nini hautaki kula? Kwa nini una huzuni ndani ya moyo wako? Basi, mimi si bora kwako kuliko watoto kumi wa kiume?”
Hana na Eli9Siku moja, walipokuwa wamemaliza kula na kunywa katika nyumba ya Yawe kule Shilo, Hana akasimama. Wakati ule, kuhani Eli alikuwa ameikaa kwenye kiti karibu na mulango wa nyumba ya Yawe.
10Hana alikuwa na huzuni sana. Na alipokuwa anamwomba Yawe akakuwa analia kwa uchungu.
11Akafanya kiapo akisema: “Ee Yawe wa majeshi, kama tu utayaangalia mateso yangu mimi mujakazi wako, ukinikumbuka mimi, bila kunisahau, mimi mujakazi wako, ukinijalia mimi mujakazi wako mutoto mwanaume, nitakupa wewe Yawe mutoto huyo akuwe wako maisha yake yote; wembe hautapita kwenye kichwa chake hata kidogo.”
12Hana aliendelea kumwomba Yawe kwa muda murefu, na kuhani Eli akakuwa anaangalia midomo yake.
13Hana alikuwa akiomba kimoyomoyo, midomo yake ilikuwa inachezacheza, lakini sauti yake haikusikilika. Hivyo Eli akafikiri kwamba Hana amelewa.
14Kwa hiyo Eli akamwambia: “Utaendelea kulewa mpaka wakati gani? Achana na kunywa divai.”
15Lakini Hana akamujibu: “Sivyo bwana wangu. Mimi ni mwanamuke mwenye taabu sana; mimi sijakunywa divai wala kinywaji kikali, lakini nimekuwa nikimutolea Yawe yanayokuwa ndani ya roho yangu.
16Usinizanie kuwa mimi ni mwanamuke asiyefaa kitu. Kwa muda wote huu nimekuwa nikisema mahangaiko yangu na taabu yangu.”
17Halafu Eli akamwambia: “Kwenda kwa amani; naye Mungu wa Israeli akupe kile ulichomwomba.”
18Hana akasema: “Ninaomba nami mujakazi wako nipate kukubaliwa mbele yako.” Hana akaenda zake, akakula chakula na hakukuwa na huzuni tena.
Kuzaliwa kwa Samweli19Kesho yake asubui, Elekana na jamaa yake waliamuka asubui mapema, na kisha kumwabudu Yawe, walirudi kwao Rama. Elekana akalala na muke wake Hana na Yawe akamukumbuka.
20Hivyo Hana akapata mimba, akazaa mutoto wa kiume. Hana akamwita mutoto huyo Samweli, maana alisema: “Nimemwomba kwa Yawe.”
21Elekana na jamaa yake yote wakaenda tena Shilo na kumutolea Yawe sadaka ya kila mwaka na kutimiza kiapo.
22Lakini mara hii Hana hakuenda, maana alimwambia mume wake hivi: “Mara tu mutoto atakapoachishwa kunyonya, nitamupeleka kusudi awekwe mbele ya Yawe, abakie kule siku zote.”
23Mume wake Elekana, akamujibu: “Fanya unaloona linafaa. Ngojea mpaka utakapomwachisha mutoto kunyonya. Yawe afanye kiapo chako kuwa kweli.” Basi, Hana alibaki kwake, akaendelea kumulea mutoto wake mpaka alipomwachisha kunyonya.
24Alipomwachisha kunyonya alimupeleka pamoja na ngombe dume wa miaka mitatu, gunia la unga na karabia ya divai. Hana alimwingiza mutoto kwenye nyumba ya Yawe kule Shilo, naye mutoto alikuwa mudogo tu.
25Walipokwisha kuchinja yule ngombe dume, walimupeleka mutoto kwa kuhani Eli.
26Hana akamwambia: “Ee bwana wangu, kama vile unavyoishi, bwana wangu, mimi ni yule mwanamuke aliyekuwa anasimama mbele yako akimwomba Yawe.
27Nilimwomba anipe mutoto huyu, na yeye alinipa kile nilichomwomba.
28Kwa sababu hiyo, mimi ninamupa Yawe mutoto huyu; wakati wote atakapokuwa anaishi, ametolewa kwa Yawe.” Halafu, wakamwabudu Yawe pale.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.