1Yawe akamwambia Musa:
2Utwae Haruni na wana wake na zile nguo takatifu, mafuta ya kupakaa, ngombe wa sadaka kwa ajili ya zambi, kondoo dume wawili, na kitunga cha mikate isiyotiwa chachu.
3Kisha, ukusanye Waisraeli wote pamoja mbele ya mulango wa hema la mukutano.
4Musa akafanya kama vile alivyoamuriwa na Yawe. Akakusanya Waisraeli wote pamoja mbele ya mulango wa hema la mukutano.
5Musa akawaambia: Hili ndilo jambo ambalo Yawe ameamuru lifanyike.
6Halafu Musa akawaleta Haruni na wana wake na kuwanawisha.
7Kisha akamuvalisha Haruni koti na kuifunga kwa mukaba, akamuvalisha kanzu, akamuvalisha kizibao na kukifunga kwenye kiuno chake kwa mukaba uliofumwa kwa ufundi.
8Kisha akaweka kifuko kwenye kifua cha Haruni na ndani ya kifuko hicho akatia mawe ya sheria. Ang. Kut 28
9Halafu akamuvalisha Haruni kofia na upande wa mbele wa Kofia hiyo akaweka pambo la zahabu, taji takatifu, kama vile Yawe alivyomwamuru.
10Kisha Musa akatwaa mafuta ya kupakaa, akaipakaa ile hema na vitu vyote vilivyokuwa ndani yake akavitakasa.
11Akanyunyiza sehemu ya mafuta hayo juu ya mazabahu mara saba, akaipakaa mafuta na vyombo vyake vyote, birika na tako lake kwa kuvitakasa.
12Vilevile Musa akamupakaa Haruni mafuta juu ya kichwa kwa kumutakasa.
13Kisha Musa akawaleta wana wa Haruni akawavalisha koti na kuwafunga mikaba kwenye viuno, na kuwavalisha kofia kama vile alivyoamuriwa na Yawe.
14Kisha Musa akaleta ngombe wa sadaka kwa ajili ya zambi, naye Haruni na wana wake wakaweka mikono yao juu ya kichwa cha ngombe huyo.
15Musa akamuchinja huyo ngombe, akatwaa damu akapakaa pembe za mazabahu pande zote kwa kidole chake kwa kuitakasa. Kisha akatwaa damu iliyobaki akaimwanga chini kwenye tako la mazabahu ambayo alitakasa kwa kuifanyia ibada ya upatanisho.
16Kisha, akatwaa mafuta yote yaliyokuwa kwenye matumbotumbo yake, sehemu bora ya maini pamoja na figo zote mbili na mafuta yake na kuviteketeza juu ya mazabahu.
17Lakini nyama ya ngombe huyo, ngozi yake na mavi yake, akaviteketeza kwa moto inje ya kambi kama vile alivyoamuriwa na Yawe.
18Kisha, Musa akaleta kondoo dume wa sadaka ya kuteketezwa. Haruni na wana wake wakaweka mikono yao juu ya kichwa cha kondoo huyo.
19Musa akamuchinja na damu ya kondoo huyo akainyunyizia mazabahu pande zake zote.
20Akakata huyo kondoo vipandevipande, akaviteketeza pamoja na kichwa chake na mafuta yake.
21Kisha kusafisha matumbotumbo na miguu kwa maji, Musa akaviteketeza vyote juu ya mazabahu pamoja na sehemu zingine za huyo kondoo kama sadaka ya kuteketezwa. Hiyo ni sadaka inayotolewa kwa moto, yenye harufu ya kumupendeza Yawe. Musa akafanya kama vile alivyoamuriwa na Yawe.
22Kisha akaleta kondoo dume mwingine, kwa ajili ya utakaso. Haruni na wana wake wakaweka mikono yao juu ya kichwa cha kondoo huyo.
23Musa akamuchinja. Akatwaa damu ya kondoo huyo na kumupakaa Haruni kwenye incha ya sikio lake la kuume, kidole gumba cha mukono wake wa kuume na cha muguu wake wa kuume.
24Wana wa Haruni nao wakakuja, naye Musa akawapakaa sehemu ya damu kwenye incha za masikio yao ya kuume, vidole gumba vya mikono yao ya kuume na kwenye vidole gumba vya miguu yao ya kuume. Damu ingine akainyunyizia mazabahu pande zake zote.
25Kisha, akatwaa mafuta yote, mukia pamoja na mafuta yake, mafuta yote yanayofunika matumbotumbo, sehemu bora ya maini, pamoja na figo zote mbili, mafuta yake na paja la muguu wa kuume wa nyuma wa huyo kondoo dume.
26Kisha, kwenye kile kitunga cha mikate iliyowekwa mbele ya Yawe akatwaa mukate mumoja usiotiwa chachu, mukate mumoja wenye mafuta na mukate mumoja mudogo, akaviweka vyote juu ya vipande vya mafuta na ule muguu.
27Musa akaviweka katika mikono ya Haruni na wana wake, nao wakafanya kitambulisho cha kumutolea Yawe.
28Kisha Musa akatwaa vitu hivyo vyote kutoka mikono yao na kuviteketeza juu mazabahu pamoja na sadaka ya kuteketezwa. Hii ni sadaka ya utakaso, yenye harufu ya kumupendeza Yawe, ni sadaka inayotolewa kwa moto.
29Kisha Musa akatwaa kile kilali na kufanya kitambulisho cha kumutolea Yawe. Sehemu hiyo ya yule kondoo dume wa utakaso ni mali ya Musa kama vile alivyoamuriwa na Yawe.
30Halafu Musa akatwaa mafuta ya kupakaa na damu kutoka mazabahu akamunyunyizia Haruni na wana wake hata na nguo zao vilevile. Hivyo Musa akamutakasa Haruni na wana wake pamoja na nguo zao.
31Musa akamwambia Haruni na wana wake: Mupike ile nyama mbele ya mulango wa hema la mukutano, muikulie pale kwenye mulango pamoja na mukate kutoka katika kitunga chenye sadaka za utakaso. Mufanye kama vile nilivyoamuriwa na Yawe, kwamba sehemu hiyo itakuliwa na Haruni na wana wake.
32Nyama yoyote au mukate wowote utakaobakia unapaswa kuteketezwa.
33Hamutatoka inje ya mulango wa hema la mukutano kwa muda wote wa siku saba, ni kusema mpaka muda wenu wa kutakaswa umekwisha, muda ambao utatwaa siku saba.
34Yawe ameamuru tufanye kama vile tulivyofanya leo kusudi tuwafanyie ibada ya upatanisho.
35Mutabaki kwenye mulango wa hema la mukutano usiku na muchana kwa muda wa siku saba, mukifanya mambo Yawe aliyoamuru, kama sivyo mutakufa. Ndivyo nilivyoamuriwa na Yawe.
36Basi, Haruni na wana wake wakafanya mambo yote Yawe aliyoamuru kwa njia ya Musa.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.