Kutoka 20 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Amri kumi(Kumb 5.1-21)

1Mungu alisema maneno haya yote:

2Mimi ni Yawe, Mungu wako, niliyekutoa katika inchi ya Misri, ambako ulikuwa mutumwa.

3Usikuwe na miungu mingine isipokuwa mimi.

4Usijifanyie sanamu ya miungu, wala mufano wa kitu chochote kinachokuwa juu mbinguni, wala kinachokuwa chini katika dunia, wala kinachokuwa ndani ya maji chini ya dunia.

8Usisahau kuiweka takatifu siku ya Sabato.

13Usiue.

14Usizini.

15Usiibe.

16Usimushuhudie mwenzako uongo.

17Usitamani nyumba ya mwenzako, wala muke wake, wala mutumwa wake au mujakazi wake, wala ngombe wake, wala punda wake, wala kitu chochote mwenzako anachokuwa nacho.

18Watu waliposikia ngurumo na kuona umeme ukiwaka na kusikia sauti ya baragumu juu ya mulima uliokuwa unafuka moshi, wote wakaogopa na kutetemeka. Wote wakasimama mbali, Ang. Ebr 12.18-19

19wakamwambia Musa: Sema nasi wewe mwenyewe, nasi tutakusikiliza. Lakini Yawe asiseme nasi, tusikufe.

20Musa akawaambia: Musiogope, maana Mungu amekuja kuwapima kusudi mupate kumwogopa siku zote na musitende zambi.

21Watu wote wakasimama mbali wakati Musa alipokaribia lile wingu zito Mungu alimokuwa.

22Yawe akamwambia Musa: Uwaambie Waisraeli: Mumejionea ninyi wenyewe kwamba nimeongea nanyi kutoka mbinguni.

23Mutaniheshimu mimi peke yangu wala musijifanyie miungu ya feza wala ya zahabu.

24Ninyi mutanijengea mazabahu ya udongo. Juu yake mutanitolea kondoo wenu na ngombe wenu kama sadaka za kuteketezwa kwa moto na sadaka za amani. Pahali popote nitakapowakumbusha watu jina langu, pale pale mimi mwenyewe nitawafikia na kuwabariki.

25Kama mukinijengea mazabahu ya mawe, musiitengeneze kwa mawe ya kuchonga, maana mukitumia vyombo vya kuchonga mawe, mutaichafua. Ang. Kumb 27.5-7; Yos 8.31

26Wala musitengeneze mazabahu yenye ngazi za kupandia, mutu asipate kuona uchi wa yule anayepanda juu yake.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help