1Nyuma ya tukio hilo, Abusaloma alijipatia gari, farasi na watu makumi tano wa kumutangulia.
2Abusaloma alizoea kuamuka asubui mapema na kwenda kusimama kwenye njia inayoelekea kwenye mulango wa muji. Mutu yeyote aliyekuwa na mashitaki ambayo alitaka kuyapeleka kwa mufalme kwa kupata uamuzi wake, Abusaloma alimwita mutu yule pembeni na kumwuliza: “Unatoka katika muji gani?” Kama mutu yule akisema ametoka katika muji fulani wa kabila la Waisraeli,
3Abusaloma alimwambia: “Maneno yako ni ya haki kabisa. Lakini hakuna mutu yeyote aliyechaguliwa na mufalme kwa kukusikiliza.”
4Tena, Abusaloma alimwambia: “Ingekuwa heri mimi ningekuwa mwamuzi wa Waisraeli! Kila mutu mwenye mashitaki au shauri angekuja kwangu, nami ningemupa haki yake!”
5Zaidi ya hayo, Abusaloma alinyoosha mukono wake akamukumbatia na kumubusu mutu yeyote aliyekuja kuinama mbele yake.
6Basi, hivi ndivyo Abusaloma alivyowatendea Waisraeli wote waliokuja kutafuta uamuzi wa mufalme. Kwa kufanya hivyo, Abusaloma aliiteka mioyo ya Waisraeli.
7Nyuma ya miaka mine, Abusaloma alimwambia mufalme: “Tafazali, uniruhusu niende kule Hebroni kwa kutimiza kiapo changu ambacho nilimwekea Yawe.
8Maana, mimi mutumishi wako, nilipoishi kule Gesuri katika inchi ya Aramu, nilimufanyia Yawe kiapo nikisema kama Yawe akinirudisha Yerusalema basi, nitamwabudu yeye.”
9Mufalme akamwambia: “Basi, kwenda kwa amani.”
Abusaloma akaondoka kwenda Hebroni.
10Lakini Abusaloma alituma wajumbe kwa siri katika makabila yote ya Waisraeli, wakasema: “Mara moja mutakaposikia mulio wa baragumu, museme: ‘Abusaloma ni mufalme katika Hebroni!’ ”
11Abusaloma alipokwenda kule Hebroni, alikwenda na watu mia mbili aliowaalika kutoka Yerusalema, nao walikwenda kule kwa nia njema, wala hawakujua kitu chochote juu ya mupango wa Abusaloma.
12Wakati Abusaloma alipokuwa akitoa sadaka, alituma ujumbe katika muji wa Gilo kwa kumwita Ahitofeli wa muji wa Gilo, aliyekuwa mushauri wa mufalme Daudi. Uasi wa Abusaloma ukazidi kupata nguvu na watu waliojiunga naye wakazidi kuongezeka.
Mufalme Daudi anatoroka toka Yerusalema13Mujumbe mumoja akamwendea Daudi na kumwambia: “Watu wa Israeli wamevutwa na Abusaloma!”
14Basi, Daudi akawaambia watumishi wake waliokuwa naye Yerusalema: “Musimame tukimbie, kama sivyo, hatutaweza kumuponyoka Abusaloma. Tufanye haraka kuondoka kusudi asituletee hasara na kuuangamiza muji kwa upanga.”
15Watumishi wake wakamwambia: “Sisi watumishi wako, bwana wetu mufalme, tuko tayari kufanya neno lolote unaloamua.”
16Basi, mufalme akaondoka pamoja na jamaa yake, lakini akawaacha wahabara wake kumi wakishugulika na kazi za nyumba.
17Mufalme akaondoka pamoja na watu wake wote. Lakini akasimama kidogo walipofikia nyumba ya mwisho katika muji.
18Watumishi wote wa mufalme, Wakereti wote, Wapeleti wote, pamoja na Wagati mia sita waliomufuata mufalme Daudi kutoka muji wa Gati waliondoka pamoja naye wakimutangulia.
19Kisha, mufalme Daudi alipomwona Itayi wa Gati, alimwambia: “Kwa nini hata wewe umeondoka pamoja nasi? Rudi ukae na yule mufalme kijana. Maana wewe ni mugeni huku, tena ni mukimbizi kutoka kwenu.
20Wewe ulikuja huku juzijuzi tu. Nikufanye mutu wa kutangatanga pamoja nasi, nikijua kwamba sijui hata kule ninakokwenda? Rudi pamoja na wandugu zako. Naye Yawe akuonyeshe wema na uaminifu.”
21Lakini Itayi akamujibu mufalme: “Kama vile Yawe anavyoishi na kama vile bwana wangu mufalme anavyoishi, popote utakapokuwa, ikiwa ni kwa kufa au ni kwa kuishi, nami mutumishi wako nitakuwa pale.”
22Basi, Daudi akamwambia Itayi: “Kwenda basi, endelea mbele.”
Hivyo, Itayi wa Gati akapita yeye mwenyewe pamoja na watoto wake.
23Daudi alipokuwa akipita pamoja na watu wake, watu wote katika inchi yote walilia kwa sauti. Mufalme Daudi akavuka kijito cha Kidroni pamoja na watu wote, wakapita kuelekea katika jangwa.
24Kuhani Abiatari akatoka, hata na kuhani Zadoki akatoka pamoja na Walawi wote wakilibeba Sanduku la Agano la Mungu. Wakaliweka lile Sanduku la Mungu chini, mpaka watu wote walipopita kutoka Yerusalema.
25Kisha mufalme akamwambia Zadoki: “Urudishe Sanduku la Agano la Mungu katika muji. Kama nimepata kukubaliwa mbele ya Yawe, bila shaka atanirudisha na kunijalia kuliona tena Sanduku lake na kuyaona makao yake.
26Lakini ikiwa Yawe hapendezwi nami basi, mimi niko tayari; na anitendee sawa vile anavyotaka.”
27Mufalme Daudi akamwambia tena Zadoki: “Twaa mwana wako Ahimasi na Yonatani mwana wa Abiatari, murudi katika muji kwa amani.
28Lakini nitakuwa nikingojea penye vivuko huku katika mbuga, mpaka nitakapopata habari kutoka kwako.”
29Kwa hiyo Zadoki na Abiatari wakalirudisha Sanduku la Agano la Mungu Yerusalema, wakabaki humo.
30Lakini Daudi aliendelea, akapanda kwenye mulima wa Mizeituni akilia, bila viatu na kichwa chake kimefunikwa. Hata watu wote waliokuwa pamoja naye walifunika vichwa vyao, wakapanda mulima wakilia.
31Wakati ule, Daudi aliambiwa kwamba hata Ahitofeli alikuwa mumoja wa waasi waliojiunga na Abusaloma. Lakini Daudi akaomba akisema: “Ee Yawe, ninakuomba uyafanye mashauri ya Ahitofeli yasifanikiwe.”
32Daudi alipofika kwenye kichwa cha mulima, nafasi ya kumwabudia Mungu, mutu mumoja jina lake Husai kutoka inchi ya Arki alikuja kwa kumupokea, nguo zake zikiwa zimepasuka na juu ya kichwa chake kuna mavumbi.
33Daudi akamwambia: “Ukienda pamoja nami, utakuwa muzigo kwangu.
34Urudi Yerusalema na kumwambia Abusaloma: ‘Nitakuwa mutumishi wako, ee mufalme, kama vile nilivyokuwa zamani mutumishi wa baba yako’. Kwa njia hiyo utanisaidia kupinga mashauri ya Ahitofeli.
35Makuhani Zadoki na Abiatari wako pamoja nawe katika muji. Basi, chochote utakachosikia kutoka katika nyumba ya mufalme, uwaambie makuhani Zadoki na Abiatari.
36Watoto wao wawili wanaume, Ahimasi mwana wa Zadoki na Yonatani mwana wa Abiatari, wako pamoja nao. Na neno lolote mutakalosikia mutanipasha habari kwa njia yao.”
37Basi, Husai, rafiki ya mufalme Daudi, akarudi katika muji wakati Abusaloma alipokuwa anaingia Yerusalema.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.