1Siku moja Samusoni akakwenda katika muji wa Gaza, akakutana na kahaba mumoja akalala naye.
2Watu wa Gaza walipoambiwa kwamba Samusoni yuko kule, wakalizunguka eneo hilo na kumuvizia kwenye mulango wa muji usiku kucha. Wakakaa kimya kule kwenye mulango usiku wote wakifikiri kwamba wanaweza kungojea mpaka mapambazuko wapate kumwua.
3Lakini Samusoni akabaki katika muji mpaka saa za usiku kati. Wakati wa usiku kati akaamuka akashika miimo miwili ya mulango, akaiongoa pamoja na vifungio vyake akaibeba na kwenda nayo mpaka karibu na Hebroni.
Delila anamutoa Samusoni4Nyuma ya mambo hayo, Samusoni akamupenda mwanamuke mumoja aliyeitwa Delila ambaye aliishi katika bonde la Soreki.
5Wakubwa wa Wafilistini wakamwendea Delila, wakamwambia: “Umubembeleze Samusoni kusudi ujue asili ya nguvu zake nyingi kusudi tuweze kumukamata na kumufunga. Ukifanya hivyo, kila mumoja wetu atakupa vikoroti makumi tatu vya feza.”
6Delila akamwambia Samusoni: “Tafazali, uniambie asili ya nguvu zako, na jinsi gani mutu anaweza kukushinda na kukufunga.”
7Samusoni akamujibu: “Wakinifunga kwa kamba saba mbichi za upinde, nitakuwa zaifu kama mutu yeyote.”
8Wakubwa wa Wafilistini wakamuletea Delila kamba hizo saba mbichi za upinde, naye akamufunga Samusoni kwa kamba hizo.
9Delila alikuwa ameweka watu wamuvizie katika chumba cha ndani. Kisha, akamwambia Samusoni kwa sauti kubwa: “Samusoni! Wafilistini wanafika kukushambulia.” Samusoni akazikata kamba hizo kama nyuzi za kitani zinapogusa moto. Hivyo hakuna aliyegundua siri ya nguvu zake.
10Delila akamwambia Samusoni: “Wewe umenichekelea. Umenidanganya. Tafazali, uniambie jinsi unavyoweza kufungwa.”
11Samusoni akamujibu: “Wakinifunga kwa kamba nyipya ambazo hazijatumiwa, nitakuwa zaifu kama mutu yeyote.”
12Basi, Delila akatwaa kamba nyipya, akamufunga nazo. Kisha akamwambia Samusoni kwa sauti kubwa: “Samusoni! Wafilistini wanakuja kukushambulia!” Wakati ule kulikuwa watu ndani ya chumba wakimuvizia. Samusoni akazikata kamba hizo kama uzi.
13Delila akamwambia Samusoni: “Mpaka sasa ungali unanichekelea. Umenidanganya. Uniambie namna wanavyoweza kukufunga.” Samusoni akamwambia: “Ukisuka nywele zangu kwa misuko saba na nyuzi ukitumia chombo cha kufuma nguo na kuvikaza kabisa kwa musumari, nitakuwa zaifu kama mutu yeyote.”
14Wakati Samusoni alipokuwa analala Delila akasuka nywele za Samusoni kwa misuko saba na nyuzi, akazifunga kwa chombo cha kufuma nguo na kukaza kabisa kwenye musumari. Kisha akamwambia Samusoni: “Samusoni! Wafilistini wanakuja kukushambulia.” Samusoni akaamuka kutoka katika usingizi akauongoa ule musumari na kutatua kile chombo cha kufuma nguo.
15Delila akamwambia Samusoni: “Unaweza namna gani kusema kwamba unanipenda na moyo wako hauko pamoja nami? Umenichekelea sasa mara tatu. Haujaniambia asili ya nguvu zako iko wapi.”
16Delila alipoendelea kumusumbua sana Samusoni kwa maneno, siku kwa siku na kumwuzi hata akachoka ndani ya roho karibu kufa,
17hakuweza kuvumilia, akamufunulia siri yake, akisema: “Nywele zangu hazijapata kunyolewa hata kidogo. Mimi nimewekwa Munaziri wa Mungu tangu katika tumbo la mama yangu. Kama nikinyolewa nguvu zangu zitanitoka, nami nitakuwa zaifu kama mutu yeyote.”
18Basi, Delila alipoona kwamba Samusoni amemwambia siri yake yote, akawaita wakubwa wa Wafilistini, akawaambia: “Mukuje mara hii moja tu maana Samusoni ameniambia siri yake yote.” Wakubwa wa Wafilistini wakamwendea Delila na walikuwa wanamuletea feza walizomwahidi.
19Naye Delila akamufanya Samusoni alale usingizi juu ya magoti yake, akamwita mutu amunyoe ile misuko yake saba. Kisha Delila akaanza kumutesa Samusoni kwa sababu sasa nguvu zilikuwa zimemutoka.
20Delila akamwambia Samusoni: “Samusoni! Wafilistini wanakuja kukushambulia!” Samusoni akaamuka toka katika usingizi naye akifikiri kwamba atatoka na kujiokoa kama vile mbele. Kumbe hakujua kwamba Yawe alikuwa amemwacha.
21Wafilistini wakamukamata, wakamwongoa macho, wakamupeleka Gaza, wakamufunga kwa minyororo ya shaba, na kumulazimisha kufanya kazi ya kusaga unga kule katika kifungo.
22Lakini nywele zake zikaanza kuota tena nyuma ya kunyolewa.
Kifo cha Samusoni23Wakubwa wa Wafilistini wakakusanyika kwa kusherehekea na kumutolea mungu wao anayeitwa Dagoni sadaka. Basi, wakakuwa wanaimba: “Mungu wetu amemutia adui yetu Samusoni katika mikono yetu.”
24Watu walipomwona Samusoni wakamusifu mungu wao na kusema: “Mungu wetu amemutia adui yetu katika mikono yetu ambaye alikuwa akiharibu inchi yetu na kuwaua wengi kati yetu.”
25Walipojaa na furaha sana ndani ya mioyo yao, wakasema: “Mulete Samusoni atuchekeshe.” Basi wakamutosha Samusoni katika kifungo, wakamuleta naye akawachekesha. Wakamuweka katikati ya nguzo.
26Samusoni akamwambia kijana aliyekuwa anamwongoza: “Uniruhusu nizipapase nguzo zinazotegemeza chumba hiki kusudi nami niziegemee.”
27Nyumba hiyo ilikuwa imejaa watu: wakubwa wote wa Wafilistini walikuwa mule na kwenye paa kulikuwa watu elfu tatu wanaume na wanawake, wakimutazama Samusoni akiwachekesha.
28Hapo Samusoni akamwomba Yawe: “Bwana wangu Yawe, ninakuomba unikumbuke. Unitie nguvu, mara hii moja tu, ee Mungu, kusudi niwalipize kisasi mara moja hii tu Wafilistini ambao waliyaongoa macho yangu mawili.”
29Samusoni akazishika nguzo mbili za katikati ambazo zilitegemeza uzito wote wa nyumba ile, mukono mumoja nguzo hii na mukono mwingine nguzo ya pili.
30Kisha akasema: “Na nikufe pamoja na Wafilistini.” Akasukuma kwa nguvu zake zote. Nyumba ikawaangukia wakubwa hao wote wa Wafilistini waliokuwa mule ndani. Wale waliouawa wakati wa kifo chake walikuwa wengi kuliko wale aliowaua wakati alipokuwa muzima.
31Wandugu zake na jamaa yake yote wakakuja kubeba maiti yake. Wakamuzika katikati ya muji wa Zora na muji wa Estaoli katika kaburi la Manoa, baba yake. Samusoni alikuwa mwamuzi wa Israeli kwa miaka makumi mbili.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.