1Yesu akatoka kule, akaenda katika muji wake wa kuzaliwa, nao wanafunzi wake wakamufuata.
2Siku ya Sabato ilipotimia, akaanza kufundisha katika nyumba ya kuabudia. Watu wengi waliomusikiliza, wakashangaa sana na kuulizana: “Huyu amepata maneno haya yote kutoka wapi? Ni hekima ya namna gani aliyopata? Ni kwa uwezo wa namna gani anafanya miujiza kama hii?
3Huyu si yule museremala, mwana wa Maria, ndugu ya Yakobo, Yose, Yuda na Simoni? Nao wadada zake, si wanaishi hapa kati yetu?” Na kwa hiyo wakakosa kumwaminia.
4Lakini Yesu akawaambia: “Nabii hakosewi heshima fasi zote, isipokuwa tu katika muji wake, katikati ya wandugu zake na katika jamaa yake.”
5Kwa hiyo Yesu hakuweza kufanya muujiza wowote kule, isipokuwa aliweka mikono yake juu ya wagonjwa wachache na kuwaponyesha.
6Naye alishangaa sana kwa sababu ya kutokuamini kwa watu wale.
Yesu anawatuma wanafunzi kumi na wawili(Mat 10.5-15; Lk 9.1-6)Kisha Yesu akazunguka katika vijiji vya kandokando akiwafundisha watu.
7Aliwaita wanafunzi wake kumi na wawili, akaanza kuwatuma wawili wawili na kuwapatia uwezo wa kufukuza pepo.
8Akawaagiza: “Musibebe kitu chochote kwa safari yenu isipokuwa fimbo tu. Musibebe chakula, mufuko, wala feza ndani ya mikaba yenu.
9Muvae viatu lakini musivae kanzu mbili.”
10Akawaambia tena: “Nafasi yoyote watakapowakaribisha ndani ya nyumba, mubakie mule mpaka mutakapotoka kule.
11Na nafasi yoyote watu watakapokataa kuwakaribisha na kuwasikiliza, mutoke kule na mukungute mavumbi toka juu ya miguu yenu. Jambo hili litakuwa ushuhuda juu yao.”
12Basi wanafunzi wakaondoka, wakahubiri watu kwamba wageuke toka zambi zao.
13Wakafukuza pepo wengi, na wakapakaa wagonjwa wengi mafuta na kuwaponyesha.
Kufa kwa Yoane Mubatizaji(Mat 14.1-12; Lk 9.7-9)14Mufalme Herode alisikia habari za Yesu, kwa maana jina lake lilikuwa limevuma fasi zote. Watu wamoja walisema: “Huyu ni Yoane Mubatizaji aliyefufuka! Ni kwa sababu hii amepata uwezo wa kufanya miujiza.”
15Lakini wengine walisema: “Huyu ni nabii Elia.” Wengine walisema: “Yeye ni nabii sawa na mumoja wa wale manabii wa zamani.”
16Lakini Herode aliposikia habari zile, akasema: “Ni yule Yoane Mubatizaji niliyemukata kichwa ndiye amefufuka!”
17Ni Herode mwenyewe aliyeamuru kwamba Yoane akamatwe na kutiwa katika kifungo. Ilitokea vile kwa sababu Herode alimwoa Herodia, muke wa ndugu yake Filipo.
18Yoane alikuwa amemwambia kwamba hana sheria ya kumwoa yule muke wa mudogo wake.
19Kwa hiyo Herodia akamuwekea Yoane chuki na kutaka kumwua, lakini hakuweza kwa sababu ya Herode.
20Herode alimwogopa Yoane, kwa sababu alijua kwamba Yoane ni mwenye haki na mutakatifu. Kwa hivi alimulinda. Alipenda kumusikiliza, ijapokuwa alifazaika sana kila mara alipomusikia.
21Siku moja Herodia alipata wakati wa kumwua Yoane. Ilikuwa sikukuu ya kuzaliwa kwa Herode, wakati alipofanya karamu kwa wasimamizi wa serikali yake, wakubwa wa waaskari na waheshimiwa wa Galilaya.
22Binti ya Herodia aliingia na kucheza hata Herode na waalikwa wake wakapendezwa. Halafu mufalme akamwambia yule binti: “Uniombe kitu chochote unachotaka, nami nitakupa.”
23Kisha akamwapia, akisema: “Nitakupa chochote utakachoniomba, hata ikiwa nusu ya ufalme wangu.”
24Basi yule binti akatoka na kwenda kumwuliza mama yake: “Niombe nini?”
Mama yake akamujibu: “Omba kichwa cha Yoane Mubatizaji.”
25Mara moja yule binti akarudi upesi kwa mufalme na kumwomba: “Ninataka unipe sasa hivi kichwa cha Yoane Mubatizaji katika sahani.”
26Mufalme akahuzunika sana, lakini hakumukatalia kwa sababu ya viapo alivyovitoa na kwa sababu ya waalikwa wake.
27Mara moja mufalme akamutuma mumoja wa waaskari wake walinzi na kumwamuru aende kuleta kichwa cha Yoane Mubatizaji. Yule askari akaenda ndani ya kifungo na kumukata Yoane kichwa.
28Kisha akakileta katika sahani, akamupa yule binti, naye akakipatia mama yake.
29Wakati wanafunzi wa Yoane walipopata habari ile, wakaenda kubeba maiti yake na kuizika.
Yesu anakulisha watu elfu tano(Mat 14.13-21; Lk 9.10-17; Yn 6.1-14)30Mitume wakarudi kwa Yesu, na kumwelezea mambo yote waliyofanya na yote waliyofundisha.
31Watu waliomufikia Yesu na kuondoka walikuwa wengi sana hata yeye na wanafunzi wake hawakupata wakati wa kula. Kwa sababu hii aliwaambia wanafunzi: “Twende peke yetu kwa pahali penye ukiwa kusudi mupumzike kidogo.”
32Basi wakaenda peke yao ndani ya chombo kwa pahali penye ukiwa.
33Lakini watu wengi waliwaona wakiondoka, wakawatambua. Kwa hiyo wakaenda kule mbio kwa miguu toka miji yote, wakawatangulia kule walipokuwa wakienda.
34Wakati Yesu alipotoka ndani ya chombo, akaona kundi kubwa la watu, akawasikilia huruma, kwa sababu walikuwa kama kondoo wasiokuwa na muchungaji. Basi akaanza kuwafundisha maneno mengi.
35Ilipofika saa za magaribi, wanafunzi wa Yesu wakamufikia na kumwambia: “Hapa ni pori na sasa ni magaribi.
36Uwaage watu hawa kusudi waende kwenye nyumba kule katika mbuga na katika vijiji vya hapa karibu wapate kujinunulia chakula.”
37Yesu akawajibu: “Ninyi wenyewe muwape chakula.”
Lakini wakamwuliza: “Unataka tuende kununua mikate kwa bei ya vikoroti mia mbili vya feza?”
38Naye Yesu akawauliza: “Muko na mikate ngapi? Muende kwanza kuangalia.”
Walipokwisha kujua, wakamwambia: “Tuko na mikate mitano na samaki mbili.”
39Basi Yesu akawaamuru wanafunzi wake wawaambie watu wote waikae chini kwenye majani kwa makundi mbalimbali.
40Wakaikaa kwa makundi ya watu mia moja mia moja, na makumi tano tano.
41Kisha Yesu akatwaa ile mikate mitano na samaki mbili, akainua macho mbinguni, akamushukuru Mungu. Akamega ile mikate, akawapa wanafunzi wake pamoja na zile samaki mbili kusudi waigawanyie watu wote.
42Wote wakakula na kushiba.
43Kisha wanafunzi wakaokota vipande vya mikate na vya samaki vilivyobaki, wakajaza vitunga kumi na viwili.
44Hesabu ya wanaume tu waliokula ilikuwa elfu tano.
Yesu anatembea juu ya maji(Mat 14.22-33; Yn 6.15-21)45Pale pale Yesu akawalazimisha wanafunzi wake waingie ndani ya chombo na kumutangulia ngambo ingine ya ziwa la Galilaya kuelekea muji Betesaida. Kwa wakati ule alibaki akiaga lile kundi la watu.
46Kisha kuwaaga, akaenda kwenye kilima kwa kuomba.
47Giza lilipoingia, chombo kilikuwa katikati ya ziwa, na Yesu alikuwa peke yake inchi kavu.
48Aliwaona wanafunzi wake wakitaabika kwa kuendesha chombo sababu upepo ulikuwa ukiwarudisha nyuma. Basi ilipokuwa karibu na mapambazuko, Yesu akawafikia akitembea juu ya maji, akitaka kuwapita.
49Nao walipomwona akitembea juu ya maji, wakawaza kwamba ni muzimu, wakaanza kulalamika,
50kwa maana wote walimwona na kuogopa sana.
Lakini mara moja Yesu akasema nao na kuwaambia: “Mujipe moyo, ni mimi! Musiogope!”
51Kisha akaingia ndani ya chombo walimokuwa, na upepo ukakoma. Kwa hiyo wanafunzi wakashangaa sana,
52kwa maana hawakuelewa maana ya ule muujiza wa kuzidisha mikate; kwa kuwa mioyo yao ilikuwa migumu.
Yesu anaponyesha wagonjwa katika inchi ya Genezareti(Mat 14.34-36)53Walipovuka ziwa, wakafika katika inchi ya Genezareti, wakaezeka chombo kwenye kivuko.
54Walipotoka ndani ya chombo, mara moja watu wakamutambua Yesu.
55Basi wakaenda mbio wakipita katika inchi ile yote, wakaanza kumuletea wagonjwa wakibebwa juu ya vipoyi, wakamufikia Yesu popote waliposikia yuko.
56Na kila pahali Yesu alipokwenda, katika vijiji, miji, au kwenye mbuga, watu waliweka wagonjwa katika viwanja vya makutano na kumusihi awaache wagonjwa waguse hata upindo wa kanzu yake tu. Nao wote waliougusa, walipona.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.