1Ee Yawe, wewe ni mwenye haki,
ingawa nitakushitaki.
Lakini ningependa nibishane nawe juu ya mambo ya haki:
Kwa nini waovu wanafanikiwa katika mambo yao?
Mbona wote wanaodanganya wanastawi?
2Umewapanda nao wameota mizizi,
wanastawi na kuzaa matunda.
Wanakujua kwa midomo tu,
lakini mioyo yao iko mbali nawe.
3Lakini wewe ee Yawe unanijua;
umeniona na kunipima.
Unajua namna ninavyokutegemea,
uwatayarishe kwa ajili ya siku ya kuuawa.
4Mpaka wakati gani inchi itaomboleza kwa kukauka,
na nyasi za mashamba yote kunyauka?
Nyama na ndege wanakufa kwa uovu wa wakaaji wake.
Wao wanasema: Mungu hataona mwisho wetu.
5Yawe akaniambia:
Ikiwa umekimbia pamoja na wenye kukimbia kwa miguu,
nao wamekuchokesha,
basi, namna gani utaweza kushindana na farasi?
Kama unaanguka katika inchi isiyokuwa na vizuizi,
utafanya nini katika pori la Yordani?
6Hata wandugu zako, jamaa yako mwenyewe,
nao vilevile wanakudaganya;
wanakukaripia waziwazi.
Usiwaamini hata kidogo,
ingawa wanakuambia maneno mazuri.
Mungu anaiacha nyumba yake na watu wake7Yawe anasema hivi:
Nimeiacha nyumba yangu;
nimeitupa mali yangu mimi mwenyewe.
Israeli, mupenzi wangu wa moyo,
nimemutoa katika mikono ya waadui zake.
8Wachaguliwa wangu wamenigeuka,
wamekuwa kama simba katika pori,
wameningurumia mimi;
ndiyo maana ninawachukia.
9Urizi wangu umekuwa kama ndege muzuri
ambaye anashambuliwa pande zote na ndege wakali?
Muende kuwakusanya nyama wote wa pori,
muwalete wakule.
10Wachungaji wengi wameharibu shamba langu la mizabibu,
wamekanyagakanyaga chini urizi wangu;
shamba langu zuri wamelifanya jangwa.
11Wamelifanya kuwa tupu;
nalo linalilia katika ukiwa wake.
Inchi yote imekuwa jangwa,
wala hakuna mutu anayejali.
12Waangamizaji wamefika,
tokea juu ya milima yote katika jangwa.
Upanga wangu unapita kuiangamiza inchi,
toka upande mumoja mpaka mwingine,
wala hakuna mutu atakayeishi kwa amani.
13Walipanda ngano, lakini walivuna magugu;
wamejichokesha kwa bure.
Kwa sababu ya hasira kali ya Yawe,
watasikia haya juu ya mavuno yao.
Mungu na jirani za Israeli14Yawe anasema hivi juu ya jirani wabaya za watu wake: Wamegusa sehemu ya urizi wangu, niliowapatia watu wangu Waisraeli! Basi nitawaongoa kutoka katika inchi yao, na hata watu wa Yuda nitawaongoa katika inchi yao.
15Lakini kisha kuwaongoa, nitawahurumia tena; nitalirudisha kila taifa katika sehemu yake na katika inchi yake.
16Na kama watajifunza mwenendo wa watu wangu kwa moyo wote, wakiapa kwa jina langu, wakisema “Kama vile Yawe anavyoishi”, kama vile walivyowafundisha watu wangu kuapa kwa jina la mungu Bali, basi watastawi katikati ya watu wangu.
17Lakini taifa lolote ambalo halitanitii, nitaliongoa kabisa na kuliangamiza.
–Ni ujumbe wa Yawe.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.