1Neno la Yawe lilinifikia kusema hivi:
2Wewe mwanadamu! Wewe unakaa kati ya watu waasi. Wana macho lakini hawaoni; wana masikio lakini hawasikii.
4Utaondoka na muzigo wako kwa wakati wa muchana, waziwazi, mbele ya macho yao. Uondoke magaribi kama vile watu wanaokwenda katika uhamisho wanavyofanya.
5Wakiwa wanakuangalia toboa ukuta wa nyumba, upitie hapo na kwenda inje.
6Wakiwa wanakuona, ujibebeshe muzigo wako kwenye mabega na kuondoka wakati wa giza. Funika uso wako usiweze kuona unakwenda wapi. Ndivyo ninavyokufanya kuwa kitambulisho kwa Waisraeli.
7Basi, nikafanya kama nilivyoamriwa. Siku hiyo, wakati wa muchana, nikafunga muzigo wangu kama muzigo wa mutu anayekimbia. Magaribi nikatoboa ukuta na giza lilipokuwa likiingia, nikatoka, nikibeba muzigo wangu juu ya mabega, watu wote wakiniona.
8Kesho yake asubui, neno la Yawe lilinifikia kusema hivi:
9Wewe mwanadamu! Hao waasi Waisraeli hawajakuuliza maana ya kitendo ulichofanya?
10Uwaambie: Bwana wetu Yawe anasema hivi: Neno langu hili linaelekea mambo yatakayomupata mutawala wa Yerusalema na Waisraeli wote wanaoishi humo.
11Uwaambie kwamba wewe ni kitambulisho kwao; kama ulivyofanya ndivyo itakavyotendeka kwao: watakwenda katika uhamisho; watakamatwa mateka.
12Naye mutawala wao atabeba muzigo wake juu ya mabega wakati wa usiku, atatoka kupitia ukuta atakaotoboa apate kutoka; atafunika uso wake kusudi asiione inchi kwa macho yake.
13Lakini nitatandaza wavu wangu juu yake, naye atanaswa katika mutego wangu. Nitamupeleka Babeli, inchi ya Wakaldea; naye akiwa huko atakufa bila kuiona inchi hiyo.
14Wafuasi wake wote, washauri wake na waaskari wake wote, nitawasambaza inje kila upande. Nitauchomoa upanga na kuwafuatilia nyuma.
15Nitakapowasambaza kati ya mataifa mengine na inchi za mbali, halafu watatambua kwamba mimi ni Yawe.
16Lakini nitawaacha wachache waepuke vita, njaa na ugonjwa mukali; kusudi hao waweze kuwaelezea watu wa mataifa wanamoishi jinsi walivyotenda mabaya. Halafu watatambua kwamba mimi ni Yawe.
17Neno la Yawe lilinifikia kusema hivi:
18Wewe mwanadamu, kula chakula na kunywa maji yako ukitetemeka kwa hofu.
19Uwaambie watu wa inchi hii: Bwana wetu Yawe anasema hivi juu ya wakaaji wa Yerusalema ambao wangali bado katika inchi ya Waisraeli: Watakula chakula chao kwa hofu na kunywa maji yao kwa kufazaika, maana inchi yao haitakuwa na kitu, kwa sababu kila mukaaji ni mutesaji mukali.
20Miji yenye watu itateketezwa, na inchi itakuwa ukiwa. Nanyi mutatambua kwamba mimi ni Yawe.
Neno la Yawe litatimia21Neno la Yawe lilinifikia kusema hivi:
22Wewe mwanadamu: Kwa nini mezali hii inatajwa katika inchi ya Waisraeli: Siku zinakuja na kupita, lakini maono ya nabii hayatimii?
23Uwaambie kwamba Bwana wetu Yawe anasema kwamba nitakomesha mezali hiyo nao hawataitumia tena katika inchi ya Waisraeli. Uwaambie kwamba wakati umefika ambapo maono yote yatatimia.
24Maana hakutakuwa tena maono ya uongo au uaguzi kati ya Waisraeli.
25Mimi Yawe mwenyewe nitatangaza yatakayotukia. Nayo yatatukia bila kukawia. Wakati ninyi mungali munaishi, enyi watu waasi, neno nitakalosema nitalitimiza.
–Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.
26Neno la Yawe lilinifikia kusema hivi:
27Wewe mwanadamu, Waisraeli wanafikiri kwamba maono yako yanahusu siku za nyuma sana, na unabii wako unahusu nyakati za mbali sana!
28Kwa hiyo uwaambie kwamba: Bwana wetu Yawe anasema hivi: Maneno yangu yote yatatimia sasa hivi.
–Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.