1 Wafalme 15 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Mufalme Abiyamu wa Yuda(2 Sik 13.1–14.1)

1Abiyamu alianza kutawala kule Yuda katika mwaka wa kumi na nane wa utawala wa mufalme Yeroboamu mwana wa Nebati.

2Alitawala kwa muda wa miaka mitatu akiwa Yerusalema. Mama yake, ambaye alikuwa binti ya Abisaloma, aliitwa Maka.

3Abiyamu alitenda zambi zilezile baba yake alizotenda, wala hakukuwa na moyo mwaminifu kwa Yawe, Mungu wake, kama babu yake Daudi alivyokuwa.

4Hata hivyo, kwa ajili ya Daudi, Yawe alimupatia Abiyamu mwana atakayetawala nyuma yake, kuwa taa ya kuangaza Yerusalema na kuuweka imara Yerusalema.

5Yawe alifanya hivyo kwa sababu Daudi alitenda mema mbele yake na hakuenda pembeni ya maagizo ya Yawe siku za maisha yake yote, isipokuwa tu lile jambo la Uria Muhiti.

6Kulikuwa vita kati ya Rehoboamu na Yeroboamu wakati wote alipokuwa mutawala.

7Matendo mengine ya Abiyamu na yote aliyofanya yameandikwa katika Kitabu cha Mambo ya Siku za Wafalme wa Yuda. Abiyamu na Yeroboamu waliishi katika hali ya vita.

8Kwa mwisho, Abiyamu akakufa na kuzikwa katika muji wa Daudi na mwana wake Asa akatawala pahali pake.

Asa, mufalme wa Yuda(2 Sik 15.16–16.6)

9Katika mwaka wa makumi mbili wa utawala wa Yeroboamu mufalme wa Israeli, Asa alianza kutawala kule Yuda.

10Alitawala kwa muda wa miaka makumi ine na mumoja. Tate yake aliitwa Maka, binti ya Abisaloma.

11Mufalme Asa alitenda mambo yanayokuwa mema mbele ya Yawe kama vile Daudi babu yake alivyofanya.

12Aliwafukuza toka katika inchi wale wote waasherati wa kidini, akaziondoa sanamu zote ambazo babu zake walikuwa wamezitengeneza.

13Akamwondoa tate yake Maka cheo chake cha mama malkia, kwa sababu alitengeneza sanamu ya Ashera na hiyo sanamu akaivunjavunja na kuiteketeza kwenye bonde la Kidroni.

14Lakini nafasi ya kutambikia miungu juu ya vilima haikuharibiwa. Hata hivyo, yeye alikuwa na moyo mwaminifu kwa Yawe maisha yake yote.

15Alirudisha katika nyumba ya Yawe matoleo yaliyokuwa yametakaswa na baba yake, pamoja na yale yake yeye mwenyewe: vyombo vya feza, zahabu na vyombo vingine vyote.

16Mufalme Asa wa Yuda na mufalme Basha wa Israeli walikuwa na vita kati yao wakati wote walipokuwa wakitawala.

17Basha, mufalme wa Israeli, aliishambulia inchi ya Yuda na kuanza kuujenga muji wa Rama kusudi apate kuzuia mutu yeyote asitoke wala asiingie kwa Asa, mufalme wa Yuda.

18Halafu mufalme Asa akatwaa feza na zahabu yote iliyobaki katika hazina ya nyumba ya Yawe na katika hazina ya nyumba ya kifalme, akawapa watumishi wake, akawatuma Damasiki kwa Beni-Hadadi mwana wa Taburimoni, mujukuu wa Hesioni, mufalme wa Aramu, akasema:

19“Tufanye mapatano ya ushirikiano kati yangu na wewe kama vile baba yangu na baba yako walivyofanya. Angalia, nimekutumia zawadi ya feza na zahabu; kwenda uvunje mapatano ya ushirikiano unaokuwa kati yako na mufalme Basha wa Israeli, kusudi aache mashambulizi juu yangu.”

20Hapo mufalme Beni-Hadadi akakubaliana na mufalme Asa, akawatuma majemadari wake na waaskari wake kwenda kuishambulia miji ya Israeli. Nao wakateka miji Iyoni, Dani, Abeli-Beti-Maka, Kineroti yote, na inchi yote ya Nafutali.

21Mufalme Basha alipopata habari za mashambulizi hayo aliacha kuujenga muji wa Rama akaenda kukaa Tirza.

22Halafu mufalme Asa akatoa tangazo kwa watu wote wa Yuda, bila kumwacha hata mutu mumoja, wahamishe mawe ya Rama na mbao, vifaa ambavyo Basha alivitumia kwa kujenga. Kisha mufalme Asa alitumia vifaa hivyo kwa kujenga kuta za Geba, katika inchi ya Benjamina na Misipa.

23Matendo mengine yote ya Asa, ushujaa wake na miji yote aliyoijenga, yote yameandikwa katika Kitabu cha Mambo ya Siku za Wafalme wa Yuda. Wakati wa uzee wake, Asa alishikwa na ugonjwa wa miguu.

24Kisha, Asa akakufa, akazikwa katika makaburi ya kifalme, katika muji wa Daudi, naye mwana wake Yehosafati akatawala kwa pahali pake.

Nadabu, mufalme wa Israeli

25Katika mwaka wa pili wa utawala wa Asa kule Yuda, Nadabu mwana wa Yeroboamu alianza kutawala katika inchi ya Israeli. Alitawala kwa muda wa miaka miwili.

26Nadabu alitenda maovu mbele ya Yawe; alifuata mwenendo wa baba yake na kutenda zambi ileile ambayo aliwasukuma watu wa Israeli watende.

27Basha mwana wa Ahiya, wa kabila la Isakari, akamufanyia Nadabu shauri baya. Basi, wakati Nadabu na waaskari wake walipokuwa wakiushambulia muji wa Gibetoni wa Wafilistini, Basha akamwua,

28akatawala kwa pahali pake. Huo ulikuwa mwaka wa tatu wa utawala wa mufalme Asa wa Yuda.

29Mara tu alipoanza kutawala, Basha akawaua watu wote wa jamaa ya Yeroboamu; hakuacha muzima hata mutu mumoja wa jamaa ya Yeroboamu. Hiyo ilikuwa sawa na yale Yawe aliyosema kwa njia ya mutumishi wake Ahiya wa Shilo.

30Mambo haya yalifanyika kwa sababu Yeroboamu alimukasirikisha Yawe, Mungu wa Israeli, kwa zambi yake na kwa kuwasukuma watu wa Israeli watende zambi.

31Mambo mengine ya Nadabu na yote aliyofanya yameandikwa katika Kitabu cha Mambo ya Siku za Wafalme wa Israeli.

32Mufalme Asa wa Yuda na mufalme Basha wa Israeli walikuwa na vita kati yao wakati wote walipokuwa wakitawala.

Basha, mufalme wa Israeli

33Katika mwaka wa tatu wa utawala wa Asa mufalme wa Yuda, Basha mwana wa Ahiya, alianza kutawala Israeli kutoka Tirza. Alitawala kwa muda wa miaka makumi mbili na mine.

34Basha alitenda maovu mbele ya Yawe; alifuata mwenendo wa Yeroboamu na kutenda zambi ileile ambayo aliwasukuma watu wa Israeli watende.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help