Zaburi 101 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Mwenendo muzuri wa mufalme

1Zaburi ya Daudi.

Wimbo wangu unaelekea wema na haki;

ninauimba kwa heshima yako, ee Yawe.

2Nitashikamana na mwenendo mukamilifu.

Utakuja kwangu wakati gani?

Nitaishi kwa ukamilifu ndani ya nyumba yangu;

3sitavumilia hata kidogo mambo ya upuuzi.

Ninachukia matendo ya watu wapotovu,

mimi sitaambatana nayo.

4Upotovu wowote ukuwe mbali nami;

sitahusika kabisa na uovu.

5Nitateketeza yule anayemuteta mwenzake,

sitamuvumilia mwenye majivuno na kiburi.

6Nitawaangalia waaminifu katika inchi,

wapate kuishi pamoja nami.

Watu wakamilifu, ndio watakaonitumikia.

7Mwongo yeyote hatakaa ndani ya nyumba yangu;

hakuna musema uongo atakayekaa kwangu.

8Siku kwa siku nitawaangamiza waovu wote katika inchi;

nitawaangamiza wabaya wote katika muji wa Yawe.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help