1Kwa nini mataifa yanafanya fujo?
Mbona watu wanafanya shauri la bure?
2Wafalme wa dunia wanajitayarisha,
watawala wanashauriana pamoja
kumwasi Yawe na muchaguliwa wake.
3Wanasema: “Tujiondoe katika utawala wao;
tutupilie mbali minyororo yao!”
4Yule anayetawala juu mbinguni
anawachekelea na kuwazarau.
5Kisha, anawakaripia kwa kasirani
na kuwatisha kwa hasira, akisema:
6“Nimemusimika mufalme niliyemuchagua;
anatawala Sayuni, mulima wangu mutakatifu!”
7Mufalme anasema: “Nitatangaza amri ya Yawe.
Mungu aliniambia: ‘Wewe ni mwana wangu,
mimi leo nimekuwa baba yako.
8Uniombe nami nitakupa mataifa kuwa urizi wako,
na dunia nzima kuwa mali yako.
9Utawaponda kwa fimbo ya chuma,
utawavunja kama chungu cha mufinyanzi!’ ”
10Sasa, enyi wafalme, mutumie akili;
musikilize onyo hili, enyi watawala wa dunia.
11-12Mumutumikie Yawe kwa woga;
muiname mbele ya mwana wake na kutetemeka,
kusudi asikasirike, nanyi musiangamie kwa rafla;
kwa maana hasira yake inawaka haraka.
Heri wote wanaokimbilia kwake!
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.