Yoshua UTANGULIZI - Swahili Congo Revised Bible 2002
UTANGULIZIJina la kitabu hiki linatokana na mutu mwenye heshima ambaye anahusika sana katika mambo tunayosimuliwa humu, ni kusema Yoshua. Yoshua alipewa madaraka ya kuwaongoza Waisraeli nyuma ya kifo cha Musa. Aliwaongoza Waisraeli mpaka walipoinyanganya ile inchi ambayo Mungu alikuwa ameahidi kuwapa. Kitabu hiki kinaeleza jinsi Waisraeli walivyoingia katika inchi ya Kanana, wakarizi inchi hiyo na kuigawanya. Kina sehemu hizi:Sura 1-12: Kuteka Kanana.Sura 13-21: Jinsi inchi inavyogawanyiwa makabila ya IsraeliSura 22: Kurudi kwa makabila ya mashariki katika sehemu yaoSura 23: Hotuba ya Yoshua ya kuwaaga WaisraeliSura 24: Kuhakikisha agano kati ya Yawe na Waisraeli