Mika 2 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Mika na wapinzani wake

1Ole wao wanaopanga kutenda maovu,

wanaolala usiku wakikusudia mabaya!

Mara tu kunapopambazuka,

wanayatimiza maana wako na uwezo.

2Wanatamani mashamba na kuyatwaa;

wakitaka nyumba, wananyanganya.

Wanawatesa wenye nyumba na jamaa zao,

wanawanyanganya watu mali zao.

3Kwa hiyo, Yawe anasema hivi:

Ninapanga kuwaletea ninyi hasara,

ambayo hamutaweza kuiponyoka hata kidogo.

Utakuwa wakati mubaya kwenu,

wala hamutaweza kutembea kwa maringo.

4Siku hiyo watu watawasimanga kwa wimbo,

watalia na kuomboleza kwa uchungu, wakisema:

Tumeangamia kabisa;

amekamata inchi yetu,

ameiondoa katika mikono yetu.

Mashamba yetu ameyagawanya kwa wale waliotuteka.

5Kwa hiyo hamutagawanyiwa sehemu yoyote ya inchi

kati ya watu wa Yawe.

Wapinzani wa nabii

6Usituhubirie sisi.

Mambo kama hayo si ya kuhubiriwa.

Sisi hatutapatwa na hasara!

7Inafaa kusema hivyo, enyi wazao wa Yakobo?

Yawe ameacha uvumilivu wake?

Yeye anafanya mambo kama haya?

Jibu la Mika

Maneno yangu yanawafalia wenye mwenendo sawa.

8Lakini Yawe anawaambia ninyi hivi:

Munawatendea watu wangu kama adui.

Munawanyanganya watu watulivu nguo zao;

watu wanaopita kwenda zao bila wasiwasi,

na wasiokuwa na mafikiri yoyote ya vita.

9Munawafukuza wake za watu wangu

kutoka nyumba zao nzuri.

Mumewaondolea watoto wao utukufu wangu milele.

10Musimame! Muende!

Hapa hakuna tena pahali pa kupumzika!

Kwa ajili ya ukosefu wenu wa uaminifu,

maangamizi makubwa yanawangojea!

11Kama mutu angetokea akitangaza maneno matupu ya uongo

na kusema “Ninawatabiria divai na pombe kwa wingi”,

muhubiri wa namna hiyo angependwa na watu hawa!

12Lakini kweli nitawakusanya ninyi wote enyi watu wa Yakobo,

nitawakusanya enyi Waisraeli muliobaki,

niwalete pamoja kama kondoo katika zizi,

kama kundi kubwa la kondoo katika shamba la malisho;

nanyi mutakuwa kundi la watu wengi.

13Yule atakayepasua njia atawatangulia,

nanyi mutauvunja mulango wa muji na kutoka inje,

mutapita na kutoka inje.

Mufalme wenu, atawatangulia;

Yawe mwenyewe atawatangulia.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help