Malaki UTANGULIZI - Swahili Congo Revised Bible 2002
UTANGULIZIKitabu cha Malaki labda kiliandikwa katika sehemu ya kwanza ya karne ya 5 mbele ya Kristo, karibu miaka mia moja nyuma ya Waisraeli kurudi katika inchi yao kutoka katika uhamisho kule Babeli.Miaka makumi tatu au makumi tano mbele ya mahubiri ya Malaki, Waisraeli walikuwa wameitikia mwito wa manabii Hagai na Zakaria kujenga upya hekalu la Yerusalema (520-515 mbele ya Kristo). Lakini kidogokidogo tazamio lao la hali mupya chini ya uongozi wa mutawala Zerubabeli lilianza kufifia. Hali ya kidini na maisha ya haki ilianza kufifia: ibada kwa Mungu ikasahauliwa (1.6-14), makuhani wakazembea katika kazi yao, nayo sheria ya Mungu ikakuwa inazarauliwa (2.1-16). Hali hiyo ilimufanya nabii huyu Malaki kuwahimiza watu wafanye mabadiliko imara na ya kimusingi katika maisha yao kwa kuwakumbusha upendo wa Mungu (1.1-5) na vilevile kwamba azabu yake iko karibu (2.17–3.5; 3.13–4.6). Aliwatangazia kwamba Mungu atamutuma mutumishi wake (3.10) ambaye atakuwa nabii kama Elia (4.5). Katika Habari Njema za Agano Jipya, ahadi hiyo inaonyeshwa kukamilika katika kazi ya Yoane Mubatizaji ambaye alikuwa na mapaswa ya kutayarisha kuja kwa Yesu Kristo (angalia Mat 17.11–13; Lk 1.17).