Mika UTANGULIZI - Swahili Congo Revised Bible 2002
UTANGULIZIMika alihubiri karibu nyakati zilezile za nabii Isaya yapata miaka 750-700 mbele ya Kristo na mahubiri yake yalikuwa kwa wakaaji wa ufalme wa kusini ni kusema Yuda. Labda alikuwa mwanafunzi wa Isaya. Alikaa Moreseti, muji uliokuwa upande wa kusini-magaribi wa Yerusalema. Hali ya nyakati nabii huyu alizoishi inaonekana katika sura tano za kwanza za kitabu hiki. Alihubiri kwamba Samaria, uliokuwa muji mukubwa wa utawala wa kaskazini, ni kusema Israeli, ungeshambuliwa na kutekwa. Aliamini vilevile kwamba utawala wa Yuda ungepatwa vilevile na hasara ile ya kitaifa. Alitangaza vilevile kuharibiwa kwa hekalu, jambo ambalo wakati huo lilizaniwa kuwa haliwezekani. Katika mahubiri yake, Mika aliwashitaki zaidi wakubwa wa watu: watajiri, watawala, waamuzi, makuhani na manabii ambao waliwakosesha watu.Kati ya mambo yanayoweza kutajwa hapa kwa sababu ya lazima yake ni ahadi ya amani katika ulimwengu chini ya utawala wa Mungu (4.1-4); maneno juu ya mufalme atakayekuja – kutoka Betelehemu –maneno ambayo yanatajwa vilevile katika Agano Jipya (5.4; angalia Matayo 2.6 na Yoane 7.42) na maneno ya lazima sana ya 6.8: kitu Yawe anachotaka kutoka kwako ni hiki: Utende mambo ya haki, utende mema, na kuishi kwa unyenyekevu mbele ya Mungu wako.