1Ujumbe wa Yawe unaoelekea Israeli. Yawe aliyezitandaza mbingu, aliyeiweka misingi ya dunia na kumupa mwanadamu uzima anasema hivi:
2Nitaufanya Yerusalema kuwa kama kikombe cha divai; na mataifa yanayokuwa kandokando yake yatakunywa na kuyumbayumba kama walevi. Muji Yerusalema utakaposhambuliwa, hata miji yote ya Yuda itashambuliwa.
3Siku hiyo nitaufanya Yerusalema kuwa kama jiwe zito kwa watu wote: yeyote atakayelinyanyua atajiumiza mwenyewe. Watu wa mataifa yote katika dunia wataushambulia muji ule.
4Siku hiyo, ninasema mimi Yawe, nitamutia hofu kila farasi, na askari mupanda-farasi wake nitamufanya kuwa mwenda-wazimu. Farasi wa mataifa mengine nitawapofusha. Lakini kabila la Yuda nitalilinda.
5Kwa hiyo wakubwa wa Yuda wataambiana: “Wakaaji wa Yerusalema wamepata nguvu yao kutoka kwa Yawe wa majeshi, Mungu wao.”
6Siku hiyo, nitawafanya wakubwa wa Yuda kuwa kama chungu chenye moto mukali katika pori, kama mwenge wa moto unaowaka kati ya miganda. Watayateketeza mataifa yote yanayokuwa kandokando yao. Lakini watu wa Yerusalema wataendelea kuishi salama katika muji wao.
7Nami Yawe nitasaidia kwanza jamaa za Yuda kusudi wazao wa Daudi na wakaaji wa Yerusalema wasijione kuwa wenye utukufu zaidi kuliko watu wengine wa kabila la Yuda.
8Siku hiyo, mimi Yawe nitawalinda wakaaji wa Yerusalema. Wanaokuwa wazaifu zaidi kati yao watakuwa na nguvu kama mufalme Daudi. Wazao wa Daudi watashika usukani kwa kuwaongoza watu wa Yuda kama Mungu, au kama malaika wa Yawe.
9Siku hiyo, nitayaangamiza mataifa yote yanayotaka kuushambulia Yerusalema.
10Halafu nitawajaza wazao wa Daudi na wakaaji wa muji Yerusalema roho ya huruma na maombi, nao watamwangalia yule waliyemutoboa kwa mukuki; watamulilia kama vile mutu anavyolia kwa kifo cha mutoto wake wa pekee, au kama vile mutu anavyomulilia kwa uchungu muzaliwa wake wa kwanza. Ang. Yn 19.37; Ufu 1.7 Ang. Mat 24.20; Ufu 1.7
11Siku hiyo kutakuwa maombolezo makubwa katika Yerusalema kama vile maombolezo ya kumwomboleza Hadadi-Rimoni katika bonde la Megido.
12Inchi itaomboleza, kila ukoo utaomboleza peke yake: wanaume peke yao na wanawake peke yao, ukoo wa Daudi peke yake, ukoo wa Natani peke yake,
13ukoo wa Lawi peke yake na ukoo wa Simei peke yake.
14Jamaa zote zilizobaki zitaomboleza: wanaume peke yao na wanawake peke yao.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.