1Ukikaa kwa kula pamoja na mutawala,
usisahau hata kidogo uko pamoja na nani.
2Zuia sana hamu yako,
ikiwa wewe unapenda sana kula.
3Usitamani vyakula vyake vizuri,
maana vinaweza kukudanganya.
4Usijichokeshe na kutafuta utajiri;
acha kufikiri juu yake.
5Macho yako yatakapokuwa yanaanza tu kuuona,
nao utatoweka mara moja.
Maana hakika utajiri unaota mabawa,
unaruka na kutoweka katika anga kama tai.
6Usikule chakula cha mutu muchoyo,
wala usitamani vyakula vyake vizurivizuri,
7maana ndani ya moyo wake anahesabu unachokula.
Atakuambia: “Kula, kunywa!”
Lakini ndani ya moyo wake hayuko pamoja nawe.
8Utatapika vipande ulivyokula;
shukrani zako zote zitakuwa za bure.
9Usiseme maneno yako mbele ya mupumbafu,
maana atazarau hekima ya maneno yako.
10Usiondoe kitambulisho cha mupaka wa zamani,
wala usinyanganye mashamba ya wayatima,
11maana Mungu, Mukombozi wao, ni mwenye nguvu,
naye atatetea haki yao nawe utaonekana kuwa na kosa.
12Tumia akili yako kwa kufuata mafundisho;
tumia masikio yako kwa kusikiliza maarifa.
13Usiache kufundisha mutoto;
ukimupiga fimbo hatakufa.
14Ukimupiga fimbo,
utayaokoa maisha yake na kuzimu.
15Mwana wangu, moyo wako ukiwa wenye hekima,
moyo wangu vilevile utakuwa wenye furaha.
16Moyo wangu utashangilia,
midomo yako itakaposema maneno ya usawa.
17Moyo wako usiwaonee wivu wenye zambi,
lakini endelea kumwogopa Yawe siku zote.
18Hakika siku nzuri zitafika
na tumaini lako halitakuwa la bure.
19Sikia, mwana wangu, ukuwe na hekima;
fikiri sana jinsi unavyoishi.
20Usikuwe mumoja kati ya walevi wa divai,
wala walafi wenye kupenda nyama,
21maana walevi na walafi wataishia kuwa wamasikini.
Usingizi utawavalisha nguo za kupasukapasuka.
22Umusikilize baba yako aliyekuzaa,
wala usimuzarau mama yako akizeeka.
23Nunua ukweli, wala usiuuzishe;
nunua hekima, mafundisho na akili.
24Baba wa mutoto mwenye haki atajaa furaha;
anayezaa mutoto mwenye hekima atamufurahia.
25Uwafurahishe baba na mama yako;
mama yako aliyekuzaa afurahi.
26Mwana wangu, unisikilize kwa uangalifu,
ufuate mwenendo wa maisha yangu.
27Kahaba ni kama shimo refu;
mwanamuke mugeni ni kama kisima chembamba.
28Yeye anavizia kama munyanganyi,
anasababisha wanaume wengi kukosa uaminifu.
29Ni nani wenye taabu?
Ni nani wenye huzuni?
Ni nani wenye ugomvi?
Ni nani wenye malalamiko?
Ni nani wenye vidonda bila sababu?
Ni nani wenye macho mekundu?
30Ni wale ambao hawabanduki penye divai,
wale ambao wanatafuta divai iliyochanganywa.
31Usiitamani divai hata kwa wekundu wake,
hata kama inametameta katika kilauri,
na kushuka vizuri unapoikunywa.
32Kwa mwisho inauma kama nyoka;
inachoma kama fira mwenye sumu.
33Macho yako yataona mambo ya ajabu,
moyo wako utatoa mambo yaliyopotoka.
34Utakuwa kama mutu anayelala katikati ya bahari,
kama mutu anayelala juu ya mulingoti wa mashua.
35Utasema: “Nimepigwa, lakini sikuumia;
wamenipondaponda, lakini sikusikia kitu.
Nitaamuka saa gani
kusudi nitafute kinywaji kingine?”
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.