Kumbukumbu la Sheria 15 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Mwaka wa Sabato(Law 25.1-7)

1“Kila mwisho wa mwaka wa saba mutawasamehe wote wenye kuwa na madeni yenu.

2Hivi ndivyo mutakavyofanya: kila mumoja aliyemukopesha mwenzake, afute lile deni, wala asijaribu kumudai kwa sababu Yawe mwenyewe ameamua deni hilo lifutwe.

3Munaweza kuwadai wageni, lakini madeni yote ya wandugu zenu wenyewe mutayafuta.

4“Yawe, Mungu wenu atawabariki katika inchi anayowapa ikuwe urizi wenu. Hakuna hata mumoja atakayekuwa masikini kati yenu,

5ikiwa tu mutamutii Yawe, Mungu wenu, kwa kufuata kwa uangalifu amri ninazowapa hivi leo.

6Yawe, Mungu wenu, atawabariki kama vile alivyowaahidi. Nanyi mutayakopesha mataifa mengi, lakini ninyi hamutakopa. Vilevile mutatawala mataifa mengi, lakini mataifa hayo hayatawatawala ninyi.

7“Kukiwa masikini wa jamaa yenu katika miji ya inchi ambayo Yawe atawapa, musikuwe wachoyo na wagumu kwake.

8Pahali pake, mufungue mikono yenu na kumukopesha kwa mapenzi kiasi cha kutosha mahitaji yake.

9Muangalie wazo ovu lisiwaingie ndani ya mioyo yenu, mukisema: ‘Mwaka wa saba, mwaka wa kusamehe wadeni uko karibu’. Mukimwangalia ndugu yenu masikini na jicho baya na kukataa kumupa chochote, yeye anaweza kumulilia Yawe juu yenu na hiyo itakuwa zambi kwenu.

10Mumupe ndugu masikini kwa moyo safi bila kunungunika, maana kwa ajili ya hayo, Yawe, Mungu wenu, atawabariki katika kazi zenu zote na katika kila munalofanya.

11Wamasikini hawatakosekana katika inchi; hivyo ninawaamuru, mukuwe wenye moyo safi kwa wandugu zenu wenye mahitaji na wamasikini katika inchi yenu.

Namna ya kuwatendea watumwa(Kut 21.1-11)

12“Kama ndugu Mwebrania, mwanaume au mwanamuke, akiuzishwa kwako, atakutumikia kwa miaka sita, lakini katika mwaka wa saba, utamwacha huru.

13Nawe utakapomwacha huru, usimwache aende mikono mitupu.

14Umupe kwa moyo safi kile ambacho Yawe amekubariki nacho: kondoo, ngano na divai.

15Mukumbuke kwamba ninyi mulikuwa watumwa huko Misri na Yawe, Mungu wenu, aliwakomboa; ndiyo maana leo ninawaamuru hivyo.

16Lakini akikuambia: ‘Sitaondoka kwako’, kwa sababu anakupenda wewe na jamaa yako na anaishi vizuri kwako,

17basi, utatwaa chuma na kutoboa sikio lake mpaka chuma hicho kiingie ndani ya mulango naye atakuwa mutumwa wako milele. Utamutendea mujakazi wako namna hiyohiyo.

18Wala usione ugumu utakapomwacha huru mutumwa wako, maana, amekutumikia kwa muda wa miaka sita kwa nusu ya mushahara wa mutumishi wa kulipwa. Fanya hivyo, naye Yawe, Mungu wako, atakubariki kwa kila utakalofanya.

Wazaliwa wa kwanza wa ngombe na kondoo

19“Umutolee Yawe, Mungu wako, wazaliwa wote wa kwanza dume wa kundi lako la ngombe na kondoo. Usiwafanyizishe ngombe hao kazi na kondoo hao usiwakate manyoya.

20Kila mwaka, wewe na jamaa yako mutakula nyama hao mbele ya Yawe, Mungu wenu, pahali Yawe atakapochagua.

21Lakini nyama huyo akiwa na kilema chochote, ni kusema kiwete au kipofu, au ana kilema chochote kikubwa, usimutoe kuwa sadaka kwa Yawe, Mungu wako.

22Utakula nyama wa namna hiyo ukiwa katika muji wako; vilevile wote wanaokuwa safi na wasiokuwa safi wanaweza kumukula kama vile unavyokula paa au kulungu.

23Lakini usikule damu yake; hiyo utaimwanga chini kama vile maji.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help