Waroma 13 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Kutii wenye mamlaka

1Kila mutu anapaswa kutii wakubwa wenye mamlaka. Maana hakuna mamlaka isiyotoka kwa Mungu; nao wakubwa wanaotawala wamesimikwa na Mungu.

2Kwa hiyo yeye anayepingana na mwenye mamlaka anapinga amri ya Mungu, nao wanaofanya vile wanajiletea azabu wenyewe.

3Kwa maana wanaofanya mema hawaogopi watawala, lakini wale wanaofanya mabaya. Unataka kuishi bila kumwogopa mwenye mamlaka? Basi fanya mema naye atakusifu,

4maana yeye anamutumikia Mungu kwa faida yako. Lakini kama ukifanya mabaya, umwogope kwa sababu yeye yuko na uwezo kwa kuazibu. Yeye anamutumikia Mungu wa kuazibu wale wanaofanya mabaya.

5Kwa sababu hii ni lazima kuwatii wenye mamlaka, si kwa sababu ya kuogopa azabu ya Mungu tu, lakini tena kwa sababu ya kusongwa na zamiri.

6Kwa sababu hii vilevile munalipa kodi, maana watawala wanamutumikia Mungu wakijitoa kwa kazi ile.

7Mumupe kila mutu haki yake: mulipishaji wa kodi, mumulipe kodi; mulipishaji wa ushuru, mumulipe ushuru. Mumuheshimu anayestahili kuheshimiwa na mumutukuze anayestahili kutukuzwa.

Kuishi katika upendo

8Musikuwe na deni la mutu yeyote. Deni moja munalopaswa kuwa nalo ni kupendana. Kwa maana yule anayemupenda mwenzake ametimiza Sheria kabisa.

9Kwa hiyo amri hizi: “Usizini, usiue, usiibe, usitamani,” pamoja na zingine zote, zinafungwa katika amri hii moja: “Umupende mwenzako sawa vile unavyojipenda mwenyewe.”

10Anayemupenda mwenzake hawezi kumutendea vibaya. Basi Sheria inatimizwa kwa njia ya upendo.

Kujiweka tayari kwa kurudia kwa Kristo

11Mufanye vile, maana munajua tunaishi katika siku gani sasa. Saa ya kuamuka katika usingizi wenu imetimia, kwa maana sasa wakati wetu wa kuokolewa unakaribia kuliko vile ilivyokuwa wakati tulipoanza kuamini.

12Usiku umepita, na muchana unakaribia. Basi tutupilie mbali matendo ya giza na kuvaa silaha za kupigana nazo wakati wa mwangaza.

13Tukuwe na mwenendo muzuri unaostahili wakati wa muchana, tukijilinda na ulafi na ulevi, uasherati na uzinzi, magombano na wivu.

14Lakini Bwana Yesu akuwe kama vile silaha munayobeba, musijiachilie kuvutwa na hali yenu ya kimwili hata mutimize tamaa zake.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help