1Neno la Yawe lilimufikia Yehu mwana wa Hanani kusema hivi juu ya Basha:
2“Wewe Basha, mimi nilikuinua kutoka katika mavumbi, nikakufanya kiongozi wa watu wangu Waisraeli. Wewe umefuata mwenendo wa Yeroboamu. Uliwasukuma watu wangu Waisraeli watende zambi na kunikasirikisha kwa zambi zao.
3Sasa, nitakufagia kabisa wewe na jamaa yako. Nitaitendea jamaa yako kama vile nilivyoitendea jamaa ya Yeroboamu mwana wa Nebati.
4Mutu yeyote wa jamaa yako atakayekufia ndani ya muji, imbwa watamukula; na mutu yeyote atakayekufia katika shamba, ndege watamukula.”
5Matendo mengine ya Basha na ushujaa wake, yote yameandikwa katika Kitabu cha Mambo ya Siku za Wafalme wa Israeli.
6Nyuma ya hayo, Basha akakufa, akazikwa kule Tirza; mwana wake Ela akatawala kwa pahali pake.
7Tena, neno la Yawe lilifika kwa njia ya nabii Yehu mwana wa Hanani juu ya Basha na jamaa yake, kwa sababu ya maovu aliyotenda mbele ya Yawe. Basha alimukasirikisha Yawe kwa matendo yake; alimwiga Yeroboamu na jamaa yake na kuiletea jamaa yake maangamizi.
Ela, mufalme wa Israeli8Katika mwaka wa makumi mbili na sita wa utawala wa Asa mufalme wa Yuda, Ela mwana wa Basha alianza kutawala kule Israeli akiwa Tirza. Alitawala kwa muda wa miaka miwili.
9Jemadari wake Simuri ambaye alisimamia nusu ya kundi ya magari yake ya vita alimwasi. Siku moja, mufalme Ela alipokuwa kule Tirza katika nyumba ya Arsa aliyekuwa musimamizi wa nyumba ya kifalme, alikunywa, akalewa.
10Basi, Simuri akaingia ndani, akamwua. Kisha akatawala kwa pahali pake. Huu ulikuwa mwaka wa makumi mbili na saba wa utawala wa Asa mufalme wa Yuda.
11Mara tu alipoanza kutawala, Simuri aliwaua watu wote wa jamaa ya Basha. Hakumwacha hata mwanaume mumoja wa jamaa yake wala warafiki zake.
12Ilikuwa kama Yawe alivyosema juu ya Basha, kwa njia ya nabii Yehu.
13Mambo haya yalifanyika kwa sababu ya zambi Basha na mwana wake Ela alizotenda. Walimukasirikisha Yawe, Mungu wa Israeli, kwa kutenda zambi na kuwasukuma watu wa Israeli watende zambi kwa sanamu za miungu yao.
14Mambo mengine ya Ela na yote aliyofanya yameandikwa katika Kitabu cha Mambo ya Siku za Wafalme wa Israeli.
Simuri, mufalme wa Israeli15Simuri alitawala kule Israeli akiwa Tirza kwa muda wa siku saba. Huo ulikuwa mwaka wa makumi mbili na saba wa utawala wa Asa mufalme wa Yuda. Watu wa Israeli walikuwa wamepiga kambi kwa kushambulia muji wa Gibetoni wa Wafilistini.
16Wakati waaskari wa Israeli waliposikia kwamba Simuri aliasi na kumwua mufalme, wote wakamuweka Omuri, jemadari wa waaskari wao, kuwa mufalme wa Israeli siku ileile.
17Omuri na waaskari wake wakaondoka Gibetoni, wakaenda na kuushambulia muji wa Tirza.
18Simuri alipoona kwamba muji umekamatwa, akaingia katika munara, ndani ya nyumba ya kifalme, akaichoma kwa moto, naye akakufia mule.
19Jambo hilo lilifanyika kwa sababu ya zambi alizotenda. Alitenda maovu mbele ya Yawe; alifuata mwenendo wa Yeroboamu na kuwasukuma watu wa Israeli watende zambi.
20Matendo mengine ya Simuri na uasi wake, yote yameandikwa katika Kitabu cha Mambo ya Siku za Wafalme wa Israeli.
Omuri, mufalme wa Israeli21Sasa, watu wa Israeli waligawanyika kwa makundi mawili: kundi moja lilimutambua Tibuni mwana wa Ginati kuwa mufalme, na kundi la pili lilimutambua Omuri.
22Watu wa kundi lililomutambua Omuri, wakawazidia nguvu wale waliomutambua Tibuni mwana wa Ginati. Tibuni akakufa na Omuri akakuwa mufalme.
23Omuri alianza kutawala katika mwaka wa makumi tatu na mumoja wa utawala wa Asa mufalme wa Yuda. Alitawala kwa muda wa miaka kumi na miwili. Miaka sita alikuwa anatawala akiwa katika muji wa Tirza.
24Alinunua mulima wa Samaria kwa vikoroti elfu sita vya feza kutoka kwa mutu mumoja anayeitwa Semeri, akajenga muji wenye kuta juu yake. Muji wenyewe akauita Samaria, kwa heshima ya Semeri aliyekuwa mwenyeji wa mulima huo hapo zamani.
25Omuri alitenda maovu mbele ya Yawe. Alitenda maovu zaidi ya wale wote waliomutangulia.
26Alifuata mwenendo wa Yeroboamu mwana wa Nebati na kutenda zambi ambazo aliwasukuma watu wa Israeli watende. Akamukasirikisha Yawe, Mungu wa Israeli, juu ya kuabudu sanamu za miungu.
27Matendo mengine ya Omuri na ushujaa wake, yote yameandikwa katika Kitabu cha Mambo ya Siku za Wafalme wa Israeli.
28Nyuma ya hayo, Omuri akakufa, akazikwa kule Samaria. Mwana wake Ahabu akatawala kwa pahali pake.
Ahabu, mufalme wa Israeli29Katika mwaka wa makumi tatu na nane wa utawala wa Asa mufalme wa Yuda, Ahabu mwana wa Omuri alianza kutawala katika inchi ya Israeli. Alitawala kule Samaria kwa muda wa miaka makumi mbili na mbili.
30Ahabu alitenda maovu mbele ya Yawe kuliko wafalme wote waliomutangulia.
31Tena, zaidi ya kufuata mwenendo mubaya wa Yeroboamu mwana wa Nebati, Ahabu alimwoa Yezebeli binti ya Etibali mufalme wa Wasidoni. Akamutumikia na kumwabudu Bali.
32Alimujengea Bali hekalu kule Samaria, na ndani yake akatengeneza mazabahu ya kumutambikia.
33Vilevile, alitengeneza sanamu ya Ashera. Ahabu alitenda maovu mengi, akamukasirikisha Yawe Mungu wa Israeli zaidi ya wafalme wote wa Israeli waliomutangulia.
34Wakati wa utawala wake, Hieli wa muji wa Beteli aliujenga upya muji wa Yeriko. Na sawa kabisa na neno Yawe alilosema kwa njia ya Yoshua mwana wa Nuni, Hieli alikufiwa na muzaliwa wake wa kwanza aliyeitwa Abiramu, wakati wa kuiweka misingi ya Yeriko. Akakufiwa vilevile na mwana wake mudogo aliyeitwa Segubu, wakati wa kuweka milango ya muji wa Yeriko.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.