1Yawe akamwambia Musa:
2Mimi nimemuchagua Bezaleli mwana wa Uri mwana wa Huri, wa kabila la Yuda
3na kumujaza Roho wangu. Nimemupatia ufahamu na akili, maarifa na ufundi,
4kusudi afanye kazi za ufundi na kufanya kazi za kufua zahabu, feza na shaba.
5Nimemupatia ujuzi wa kuchonga mawe ya kupamba, kuchonga mbao, na ujuzi wa kila aina ya ufundi.
6Vilevile nimemuchagua Oholiabu mwana wa Ahisamaki wa kabila la Dani, afanye kazi pamoja naye. Vilevile nimewapa uwezo mukubwa watu wengine kwa ajili ya kazi mbalimbali, kusudi watengeneze vifaa vyote nilivyoagiza vifanywe:
7hema la mukutano, Sanduku la Agano na kiti cha ushuhuda juu yake, pamoja na vifaa vyake vyote,
8meza na vyombo vyake, kinara safi cha taa na vyombo vyake, mazabahu ya kufukizia ubani,
9mazabahu ya sadaka za kuteketezwa na vyombo vyake vyote, birika la maji pamoja na tako lake,
10nguo takatifu ya kuhani Haruni na wana wake ambao watafanya kazi ya ukuhani,
11mafuta ya kupakaa na ubani wenye harufu nzuri kwa ajili ya Pahali Patakatifu. Vitu hivyo vyote vitatengenezwa kulingana kabisa na jinsi nilivyokuamuru.
Sabato: siku ya kupumzika12Yawe akamwambia Musa:
13Uwaambie Waisraeli hivi: Ninyi mutashika hakika Sabato zangu, kwa sababu hizo ni kitambulisho kati yenu na mimi kwa vizazi vyote kwamba mimi ndimi ninayewatakasa.
14Mutashika Sabato, nayo itakuwa kwenu siku takatifu. Yeyote atakayeichafua siku hiyo anapaswa kuuawa. Na mutu atakayefanya kazi yoyote siku hiyo atatengwa mbali na watu wake.
15Mutafanya kazi zenu kwa muda wa siku sita, lakini siku ya saba ni siku ya Sabato, ni siku ya kupumzika ambayo ni takatifu kwa ajili ya Yawe. Mutu yeyote atakayefanya kazi yoyote siku hiyo lazima atauawa.
18Yawe alipomaliza kuongea na Musa juu ya mulima Sinai, akamupatia Musa vile vibao viwili vya mawe ambavyo juu yake Mungu aliziandika zile amri kwa kidole chake mwenyewe.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.