Yakobo 4 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Haifai kupenda raha za dunia

1Magombano na ugomvi vinavyokuwa kati yenu vinatoka wapi? Si vinatoka katika tamaa zenu zinazopigana ndani ya miili yenu?

2Munatamani kupata kitu fulani, lakini hamukipati. Munaua na kusikia wivu, lakini hamuwezi kupata kitu. Na kwa hiyo, munagombana na kuwa na ugomvi. Hamupati kitu munachotaka kwa sababu hamukiombi kwa Mungu.

3Wakati munapoomba, hamupati kitu kwa sababu munaomba kwa nia mbaya, kwa maana munataka vitu kusudi mutimize tu tamaa zenu.

4Ninyi watu wasiokuwa na uaminifu! Hamujui kwamba kupenda raha ya dunia ni kuwa adui wa Mungu? Basi yeye anayetaka kupenda raha za dunia anajifanya mwenyewe kuwa adui wa Mungu.

5Musizani kwamba ni kwa bure Maandiko Matakatifu yanasema: “Mungu anasikia wivu sana kwa ajili ya yule Roho aliyemuweka akae ndani yetu.”

6Lakini Mungu ametujalia neema kubwa zaidi, kwa maana Maandiko yanasema: “Mungu anapingana na wenye kiburi, lakini anawajalia wanyenyekevu neema.”

7Basi mumutii Mungu. Mupingane na Shetani, naye atawakimbia.

8Mumukaribie Mungu, naye atawakaribia. Musafishe mikono yenu, ninyi wenye zambi! Mutakase mioyo yenu, ninyi wenye nia mbili!

9Musikitike, mulie na kulalamika. Kucheka kwenu kugeuke kuwa kilio, na furaha yenu igeuke kuwa huzuni.

10Mujinyenyekeze mbele ya Bwana, naye atawainua.

Usihukumu ndugu yako

11Wandugu, musisemeane ubaya. Yule anayesema ubaya juu ya ndugu yake au kumuhukumu, anasema ubaya juu ya Sheria na kuihukumu. Ukihukumu Sheria, wewe si mwenye kutii Sheria, lakini mwenye kuihukumu.

12Mungu peke yake ndiye anayesimamisha Sheria na anayeweza kuhukumu. Ni yeye peke yake anayeweza kuokoa na kuangamiza. Basi wewe unayemuhukumu mwenzako, unajizania kuwa nani?

Si vizuri kujisifu

13Munisikilize sasa, ninyi munaosema: “Leo au kesho tutakwenda katika muji fulani, tutakaa kule kwa muda wa mwaka muzima, tutafanya biashara na kupata faida.”

14Ninyi hamujui namna gani maisha yenu yatakavyokuwa kesho! Kwa maana ninyi ni kama muvuke unaoonekana kwa wakati kidogo, kisha unatoweka.

15Ninyi mungepaswa kusema: “Kama Bwana anataka, tutaishi na kufanya hivi na hivi.”

16Lakini sasa munajivuna na kujisifu. Majivuno yote ya namna hii ni mabaya.

17Basi, mutu anayejua kutenda mema wala hayatendi, anafanya zambi.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help