Mwanzo UTANGULIZI - Swahili Congo Revised Bible 2002

UTANGULIZIKitabu cha Mwanzo kinasema juu ya kuumbwa kwa ulimwengu, asili ya wanadamu, mwanzo wa zambi na wa mateso katika dunia. Kinasema vilevile juu ya njia ya kuleta ushirika kati ya Mungu na wanadamu. Kitabu hiki kinaweza kugawanywa katika sehemu mbili kubwa:Sura 1–11: Kuumbwa kwa dunia na mwanzo wa historia ya wanadamu. Hapa kuna habari za Adamu na Eva, za Kaina na Abeli, za Noa na mafuriko ya maji, na za Munara wa Babeli.Sura 12–50: Mwanzo wa historia ya babu za Waisraeli. Babu wa kwanza ni Abrahamu ambaye alijulikana kwa njia ya imani yake na kwa utiifu wake. Kisha kunafuata habari za mwana wake Isaka, za mujukuu wake Yakobo (anayeitwa vilevile Israeli), na za wana kumi na wawili wa Yakobo ambao ndio babu za makabila kumi na mawili ya Israeli. Mukazo unatiliwa sana juu Yosefu ambaye ni mumoja kati ya wana hawa, na mambo yaliyomusukuma Yakobo na wana wake wengine pamoja na jamaa zao kwenda kuishi kule Misri.Kitabu hiki kinaanza na kuhakikisha kwamba Mungu aliumba ulimwengu na ulimwengu ulikuwa muzuri. Lakini zambi za wanadamu zikavunja ushirika wao na Mungu, na wanadamu wengine, hata na dunia. Wazo kubwa la kitabu hiki ni kwamba Mungu anataka tena kurudishia ulimwengu ile hali yake nzuri.Mambo makubwa katika kitabu hiki ni–Kuumbwa kwa ulimwengu na kwa wanadamu: sura 1–2–Mwanzo wa zambi na wa mateso: sura 3–Tangia Adamu mpaka Noa: sura 4–5–Noa na mafuriko ya maji: sura 6–10–Munara wa Babeli: sura 11–Babu: Abrahamu, Isaka, Yakobo: sura 12–35–Wazao wa Esau: sura 36–Yosefu na wandugu zake: sura 37–45–Waisraeli katika Misri: sura 46–50
Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help