Ezekieli 22 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Makosa ya Yerusalema

1Neno la Yawe lilinifikia kusema hivi:

2Ewe mwanadamu! Uko tayari kutoa hukumu, kuuhukumu muji huu wa wauaji? Basi, ujulishe machukizo yake yote.

3Uuambie kwamba:

Bwana wetu Yawe anasema hivi: Wewe ni muji unaowaua watu wako mwenyewe na kujichafua kwa kufanya sanamu za miungu; kwa hiyo wakati wako wa azabu umetimia.

4Una makosa kutokana na damu uliyomwanga. Umejichafua kwa sanamu ulizojifanyia. Umeileta siku yako ya azabu karibu nawe; siku zako zimehesabiwa. Ndiyo maana nimekufanya uchekelewe na mataifa na kuzarauliwa na inchi zote.

5Inchi zote za mbali na za karibu zitakuchekelea. Umejipatia sifa mbaya na kujaa fujo.

6Wakubwa wa Waisraeli wanaokuwa humo, kila mumoja kadiri ya nguvu zake anaua watu.

7Kwako baba na mama wanazarauliwa. Mugeni anayekaa kwako ananyanganywa mali yake. Wayatima na wajane wanaonewa.

13Nimekunja ngumi yangu juu yako kwa sababu ya hiyo faida uliyopata kwa njia isiyokuwa ya haki na kwa mauaji yaliyofanyika kwako.

14Utaweza kuvumilia kuwa hodari siku nitakapokushambulia? Ni mimi Yawe ninayesema hivyo na nitakayetimiza hayo.

15Nitakusambaza kati ya mataifa na kukutupatupa katika inchi zingine. Nitaukomesha uchafu unaokuwa ndani yako.

16Utajichafua mbele ya mataifa mengine, lakini utatambua kwamba mimi ni Yawe.

Furu la Mungu la kusafishia

17Tena neno la Yawe lilinifikia kusema hivi:

18Wewe mwanadamu! Waisraeli wamekuwa kwangu kama takataka. Wao ni kama takataka inayobaki wakati madini ya shaba, bati, chuma au risasi yanaposafishwa.

19Kwa hiyo, Bwana wetu Yawe anasema hivi: Kwa kuwa ninyi wote mumekuwa takataka ya madini, mimi nitawakusanya pamoja katika Yerusalema.

20Kama vile watu wanavyokusanya feza, shaba, chuma, risasi na bati katika furu wapate kuzisafisha kwa moto, ndivyo kasirani na hasira yangu vitakavyowakusanya huko na kuwayeyusha.

21Nitawakusanya na kuwawasha moto kwa kasirani yangu; nanyi mutayeyuka mukiwa humo ndani ya muji.

22Kama feza inavyoyeyuka katika furu, ndivyo mutakavyoyeyushwa humo katika muji. Nanyi mutatambua kwamba mimi Yawe nimeimwanga kasirani yangu juu yenu.

Zambi za wakubwa wa Waisraeli

23Neno la Yawe lilinifikia kusema hivi:

24Wewe mwanadamu! Uwaambie Waisraeli kwamba inchi yao ni kama inchi ambayo haijanyeshewa, imenyauka kwa sababu ya kasirani yangu ikakuwa kama udongo bila maji.

25Wakubwa wenu ni kama simba anayenguruma anaporarua nyama wake. Wanaua watu, wanawanyanganya watu mali na vitu vyao vya bei kali, na kuongeza hesabu ya wajane.

26Makuhani wao wanavunja sheria zangu, na kukufuru vyombo vyangu vitakatifu. Hawapambanui kati ya vitu vitakatifu na vitu visivyokuwa vitakatifu, wala hawafundishi watu tofauti kati ya mambo yanayokuwa machafu na yanayokuwa safi. Wameacha kuzishika Sabato zangu, na kunizaraulisha kati yao.

27Wakubwa wake wanaokuwa ndani ya muji ni kama imbwa wa pori wanaorarua nyama wao; wanaua kwa kujitajirisha kwa namna isiyokuwa ya haki.

28Manabii wake wanaficha maovu hayo kama mutu anapotia chokaa kwenye ukuta wenye kuharibika. Wanapata maono ya uongo na kutabiri udanganyifu mutupu, wakisema “Bwana wetu Yawe anasema hivi”, wakati mimi mwenyewe sikuwaambia chochote.

29Kila fasi katika inchi watu wanatendeana vibaya na kunyanganya kwa kinguvu. Wanagandamiza wamasikini na wakosefu, na kuwaonea wageni bila kujali.

30Nilitafuta kati yao mutu mumoja atengeneze ukuta na kusimama juu ya nafasi iliyobomoka mbele yangu, kusudi ailinde inchi na kunizuia nisiiharibu, lakini sikumupata hata mumoja.

31Kwa hiyo nimewamwangia kasirani yangu na kwa moto wa hasira yangu nimewateketeza kulingana na matendo yao. –Ndivyo anavyosema Bwana wetu Yawe.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help