ZAKARIA UTANGULIZI - Swahili Congo Revised Bible 2002
UTANGULIZIKitabu cha Zakaria kinaweza kuitwa kitabu cha matumaini. Kitabu chenyewe kina sehemu mbili. Sehemu ya kwanza (sura 1–8) ina mahubiri ya nabii yaliyotolewa kati ya mwaka 520 na 518 mbele ya Kristo. Mahubiri hayo ya kinabii mara nyingi yanafanyika kwa njia ya maono, na yanakumbusha kwamba ujenzi mupya wa hekalu na kutengenezwa kwa Yerusalema kutakuwa kitambulisho cha kufika kwa nyakati mupya za baraka. Nyakati hizo zitaanzishwa na Mungu kwa kumuchagua mutawala Zerubabeli na kuhani mukubwa Yoshua. Tumaini la Waisraeli linaelekezwa juu ya kungojea kwa hamu wakati ule Mungu atakapotawala juu ya inchi yote.Sehemu ya pili ya kitabu hiki (sura 9–14) inakumbusha mambo mawili: la kwanza ni juu ya hali na tabia za sifa za yule mutu atakayetumiwa na Mungu kwa kuanzisha utawala wa Mungu. Yule anaelezwa kama mufalme munyenyekevu na mwenye ushindi; mufalme anayekuwa kama kondoo anayepelekwa kuuawa. Katika Agano Jipya waandishi wa Injili wamerudilia tazamio lile kwa kueleza utumishi wa Yesu hasa juu ya kifo chake (ang Matayo 21.4-5; 26.31; Mk 14.27 na Yoane 19.37).