1Usiku nikiwa kwenye kitanda changu,
nilimutafuta yule ninayemupenda.
Nilimutafuta, lakini sikumupata.
2Nikaamuka, nikazunguka katika muji,
katika barabara na nafasi za makutano,
nikimutafuta yule wangu wa moyo.
Nilimutafuta, lakini sikumupata.
3Walinzi wa muji waliniona
walipokuwa wanazunguka katika muji.
Basi nikawauliza:
Mumemwona mupenzi wangu wa moyo?
4Mara tu nilipoachana nao,
nikamwona mupenzi wangu wa moyo.
Nikamushika wala sikumwacha aondoke,
mpaka nilipomupeleka katika nyumba kwa mama yangu,
mpaka ndani ya chumba cha yule aliyenizaa.
5Ninawasihi, enyi wabinti wa Yerusalema,
kama vile paa au swala wanavyokuwa katika pori,
musichochee wala kuamusha mapenzi,
mpaka pale wakati wake utakapofika.
Shairi la tatuBibi arusi6Ni kitu gani kile kinachotoka katika jangwa
kama munara wa moshi,
kinachotoa harufu ya manemane na ubani,
manukato yanayouzishwa na wachuuzi?
7Angalia! Ni kipoyi cha Solomono,
akibebwa juu ya kiti chake cha kifalme,
akizungukwa na walinzi makumi sita,
mashujaa bora wa Israeli.
8Kila mumoja wao ameshika upanga,
kila mumoja wao ni hodari wa vita.
Kila mumoja ana upanga wake kwenye kiuno,
tayari kupambana na adui usiku.
9Mufalme Solomono alijitengenezea kipoyi,
kwa mbao nzuri kutoka Lebanoni.
10Nguzo zake zilitengenezwa kwa feza,
nafasi ya kuegemea imefunikwa kwa zahabu,
nafasi ya kuikalia imefunikwa na vitambaa vya nyekundu-nyeusi.
Katikati yake kilipambwa na wabinti wa Yerusalema
waliokishonea vitambulisho vya upendo.
11Mukuje basi enyi wabinti wa Sayuni,
mumwone mufalme Solomono.
Amevaa taji aliyovalishwa na mama yake,
siku alipofanya ndoa yake,
siku ambayo moyo wake ulijaa furaha.
Masemi ya mumeWho We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.