Yobu 19 - Swahili Congo Revised Bible 2002

1Kisha Yobu akajibu:

2Mutaendelea kunitesa mpaka wakati gani,

na kunivunjavunja kwa maneno?

3Mara hizi zote kumi mumenitukana.

Basi, hamusikii haya kunitendea vibaya?

4Hata kama ingekuwa nimekosa kweli,

kosa langu linanielekea mimi mwenyewe.

5Munaishusha hali yangu mupate kujipandisha;

munanitusi kwa kunyenyekezwa kwangu.

6Mujue kwamba Mungu amenitendea vibaya

na kuninasa katika wavu wake.

7Ninalalamika: “Mateso makali!”

lakini sijibiwi.

Ninaita kwa sauti kubwa,

lakini sipati haki yangu.

8Njia yangu ameiziba kwa ukuta kusudi nisipite,

njia zangu amezitia giza.

9Amenivua utukufu wangu;

ameiondoa taji yangu juu ya kichwa.

10Amenivunja pande zote, nami nimekwisha;

tumaini langu ameliongoa kama muti.

11Ameichochea kasirani yake juu yangu;

ameniona kuwa kama adui yake.

12Majeshi yake yananifikia kwa pamoja;

yametengeneza njia ya kuja kwangu,

yamepiga kambi kuizunguka nyumba yangu.

13Mungu amewaweka wandugu zangu mbali nami;

warafiki zangu wakubwa wamenitoroka kabisa.

14Wandugu zangu na warafiki hawanisaidii tena.

15Wageni katika nyumba yangu wamenisahau;

wajakazi wangu wananiona kuwa mugeni.

Mimi nimekuwa kwao mutu wasiyemujua.

16Ninamwita mutumishi wangu lakini haitikii,

ninalazimishwa kumusihi sana kwa maneno.

17Nimekuwa harufu mbaya kwa muke wangu;

chukizo kwa wandugu zangu wa tumbo.

18Hata watoto wadogo wananizarau;

wakati ninapojitokeza wao wananizomea.

19Warafiki zangu wakubwa wanachukizwa nami,

wale niliokuwa nikiwapenda wamenigeuka.

20Mwili wangu umebakia tu mifupa na ngozi,

nimeponyoka kisha kupoteza yote.

21Munionee huruma,

munionee huruma, enyi warafiki zangu;

maana mukono wa Mungu umenigusa.

22Kwa nini munanifuatilia kama Mungu?

Mbona hamutosheki na mwili wangu?

23Heri maneno yangu yangeandikwa!

Heri yangeandikwa katika kitabu!

24Heri yangechorwa kwa chuma na risasi

juu ya jiwe kusudi yadumu!

25Ninajua wazi Mukombozi wangu anaishi.

Kwa mwisho yeye atasimama hapahapa katika dunia.

26Na nyuma ngozi yangu kuharibika hivyo,

nitamwona Mungu nikiwa na mwili huu.

27Mimi mwenyewe nitakutana naye.

Mimi mwenyewe na si mwingine nitamwona kwa macho.

Moyo wangu unachomwa kwa kumungojea.

28Ninyi munaweza kujisemesha:

“Tutamufuatilia namna gani?

Namna gani tutapata kwake maneno ya kumushitaki?”

29Lakini muogope azabu,

chuki yenu isiwaletee kifo.

Mujue kwamba kutakuwa hukumu!

Masemi ya tatu ya Zofari
Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help