1Kwa mukubwa wa waimbaji. Zaburi ya Daudi.
2Kwako, ee Yawe,
ninakimbilia.
Usiniache nifezeheke hata kidogo;
kwa haki yako, uniokoe.
3Unitegee sikio, uniokoe haraka!
Ukuwe kwangu kikingio na kimbilio,
kusudi nipate kuokoka.
4Wewe ni kikingio na upango wangu;
kwa heshima ya jina lako,
uniongoze na kunionyesha njia.
5Uniopoe katika mutego walionitegea;
maana wewe ni mulinzi wangu.
6Ninaweka roho yangu katika mikono yako;
umenikomboa, ee Yawe, Mungu mwaminifu.
7Ninawachukia wanaoabudu vitu vya bure.
Mimi, ninakutumainia wewe, ee Yawe.
8Nitashangilia na kufurahia wema wako,
maana wewe unaona taabu yangu,
unajua huzuni yangu.
9Wewe haukunitoa katika mikono ya waadui zangu;
lakini umenisimamisha kwenye pahali pa usalama.
10Unionee huruma, ee Yawe, niko katika taabu;
macho yangu yamechoka kwa ajili ya huzuni,
nimeishiwa nguvu katika mwili na roho.
11Maisha yangu yamekwisha kwa ajili ya kuugua;
nayo miaka yangu kwa ajili ya kusikitika.
Nguvu zangu zimeniishia kwa kutaabika;
hata mifupa yangu imekauka.
12Waadui zangu wote wananizarau,
na hasa zaidi wenzangu.
Warafiki zangu wameniona kuwa kitisho;
wanaponiona katika njia wananikimbia.
13Nimesahaulika kama mutu aliyekufa;
nimekuwa kama chungu kilichovunjikavunjika.
14Ninasikia watu wakinongonezana;
kuna vitisho kila upande.
Wanafanya shauri baya juu yangu,
wanafanya mipango ya kuniua.
15Lakini mimi ninakutumainia wewe, ee Yawe.
Ninasema: “Wewe ni Mungu wangu!”
16Maisha yangu ni katika mikono yako.
Uniokoe kutoka waadui zangu,
uniokoe kutoka hao wanaonitesa.
17Uniangalie mimi mutumishi wako;
uniokoe kwa wema wako.
18Usiniache nifezeheke, ee Yawe,
maana mimi ninakulilia;
lakini uwaache waovu wafezeheke,
uwaache wapotelee huko kuzimu.
19Funga midomo ya hao watu waongo,
watu wenye kiburi na majivuno,
ambao wanazarau watu wa haki.
20Kweli, mazuri yako ni mengi sana,
unayowawekea wale wanaokuabudu!
Unawatendea mazuri mbele ya watu wote
wale wanaokukimbilia.
21Unawaficha kwenye usalama pahali unapokuwa,
mbali na mipango mibaya ya watu;
unawalinda salama,
mbali na ubishi wa waadui zao.
22Yawe asifiwe,
maana amenionyesha wema wake wa ajabu,
nilipozungukwa katika muji unaoshambuliwa.
23Nami niliogopa na kuzani kwamba ulikuwa umenitupa;
kumbe, ulisikia kilio changu nilipokuita unisaidie.
24Mumupende Yawe, enyi watakatifu wake wote.
Yawe anawalinda watu waaminifu;
lakini anawaazibu kabisa wenye kiburi jinsi wanavyostahili.
25Mujitie moyo, mukuwe hodari,
enyi wote munaomutumainia Yawe.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.