1Yawe aliniambia hivi: Twaa ubao mukubwa, uandike juu yake maneno yanayosomeka waziwazi: “Teka haraka. Nyanganya Upesi.”
2Basi, nikajipatia washuhuda wawili waaminifu ambao wangenishuhudia: Kuhani Uria na Zekaria mwana wa Yeberekia.
3Nikalala na muke wangu ambaye vilevile ni nabii, akapata mimba, akazaa mutoto mwanaume. Yawe akaniambia: Umupe mutoto huyo jina “Teka-haraka-nyanganya-upesi.”
4Maana mbele mutoto huyu hajafikia umri wa kuweza kutamka neno “Baba” au “Mama”, utajiri wa muji wa Damasiki na vitu walivyonyanganya kule Samaria vitapelekwa kwa mufalme wa Asuria.
Mufalme wa Asuria anakuja5Yawe alisema nami tena, akaniambia:
6Kwa sababu watu hawa wameyakataa maji ya Siloa yanayotiririka polepole, wakatetemeka mbele ya mufalme Resini na mufalme Peka mwana wa Remalia,
7basi, Bwana wao atawaletea mafuriko makubwa ya maji ya muto Furati, ni kusema mufalme wa Asuria na nguvu zake zote; yatafurika na kupita kingo zake.
8Utaingia ndani ya inchi ya Yuda kwa nguvu na kufurika na kupanda mpaka kwenye shingo. Utaenea juu ya inchi yako yote, ee Emanueli!
Mipango ya bure ya watu9Muungane, enyi watu wa mataifa, na kufezeheshwa!
Musikilize, enyi inchi za mbali katika dunia!
Mujiweke tayari na kufezeheshwa.
Mujiweke tayari na kufezeheshwa.
10Mushauriane pamoja lakini itakuwa bure;
mufanye mipango lakini haitawezekana,
maana Mungu Yuko Pamoja Nasi.
Maonyo kwa nabii11Yawe alinionya kwa nguvu nisifuate njia za watu hawa, akaniambia:
12Musijiunge nao katika mashauri yao mabaya, wala musiogope yale wanayoyaogopa wala kuwa na hofu.
19Watu wamoja watawaambia ninyi: Muombe shauri kwa mizimu na waaguzi wanaolia kama ndege; kwa sababu ni kawaida watu kuomba shauri kwa miungu yao, na kuomba shauri kwa wafu kwa ajili ya wanaokuwa wazima.
20Hakika anayesema hivyo hajapata kuona mwangaza. Lakini ninyi mushike lile agizo na mafundisho ya Mungu.
Taabu21Watu watatangatanga katika inchi, wenye kufazaika sana na wenye njaa. Na wakiwa na njaa, watakasirika na kumulaani mufalme wao vilevile na Mungu wao. Wataangalia juu mbinguni
22na kuiangalia dunia, lakini wataona tu taabu, giza na mateso makubwa. Hakuna atakayeepuka giza hilo kubwa.
Mutoto amezaliwa kwetu23Lakini inchi ile iliyokuwa imepatwa na huzuni haitabaki siku zote katika giza hilo kubwa. Hapo zamani Mungu alizifezehesha inchi za Zebuluni na Nafutali, lakini siku zinazokuja atafanya kuwa na utukufu kandokando ya bahari, inchi inayokuwa ngambo ya Yordani, na hata Galilaya ambamo watu wa mataifa wanaishi.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.