1 Petro 5 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Maonyo kwa wazee wa kanisa

1Ninawaonya wazee wa kanisa wanaokuwa kati yenu. Mimi vilevile ni muzee mwenzenu, nami ni mushuhuda wa mateso ya Kristo na zaidi ya hii nitashiriki katika utukufu ule utakaotokea.

2Ninawaonya, muchunge lile kundi Mungu alilowapatia, si kwa kulazimishwa, lakini kwa mapenzi yenu sawa vile Mungu anavyotaka. Musitumike kwa ajili ya tamaa mbaya ya mali, lakini kwa kujitoa kwa moyo mwema.

3Musitawale kwa kinguvu kundi lile lililowekwa chini ya uangalizi wenu, lakini mukuwe mifano kwao.

4Na wakati Muchungaji Mukubwa atakapotokea, mutapokea taji ya utukufu isiyoweza kuharibika.

5Na hivi vilevile, ninyi vijana, munapaswa kuwatii hao wazee. Ninyi wote munapaswa kuwa na unyenyekevu, mupate kutumikiana; maana Maandiko Matakatifu yanasema: “Mungu anawapinga wenye kiburi, lakini anawajalia wanyenyekevu neema.”

6Basi mujinyenyekeze mbele ya Mungu mwenye uwezo, kusudi awainue kwa wakati unaofaa.

7Mumutolee masumbuko yenu yote kwa maana yeye anawashugulikia.

8Mukuwe waangalifu na mukeshe, kwa maana adui yenu Shetani anazungukazunguka kama simba anayenguruma akitafuta yule atakayerarua.

9Mupingane naye, mukisimama imara katika imani, mukijua kwamba fasi zote katika dunia, wandugu zenu wanapata mateso kama hayo.

10Lakini mukisha kuteswa kwa muda kidogo, Mungu mwenye neema yote aliyewaita kusudi mupate kushiriki naye katika utukufu wake wa milele katika kuungana kwenu na Kristo, yeye mwenyewe atawakamilisha. Atawatia nguvu na kuwasimamisha imara kabisa.

11Yeye ndiye Mungu mwenye uwezo kwa milele na milele. Amina.

Salamu za mwisho

12Nimewaandikia barua hii fupi nikisaidiwa na Sila, ninayemujua kuwa ndugu mwaminifu. Ninataka kuwatia moyo na kushuhudia kwenu kwamba mambo hayo yanayoelekea neema ya Mungu ni ya kweli; nanyi musikose kushikamana nayo.

13Kanisa linalokuwa katika Babeli, lililochaguliwa na Mungu kama vile ninyi, linawasalimia. Vilevile Marko, mwana wangu katika imani, anawasalimia.

14Musalimiane kwa upendo wa kindugu. Ninawatakia amani ninyi watu wote wa Kristo.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help