1Kwa mukubwa wa waimbaji. Zaburi ya Daudi.
2Heri mutu anayeshugulikia masikini;
Yawe atamwokoa wakati wa shida.
3Yawe atamulinda na kuchunga uzima wake,
naye atafanikiwa katika inchi;
hatamwacha katika makucha ya waadui zake.
4Yawe atamusaidia anapokuwa mugonjwa,
atamuponyesha magonjwa yake yote.
5Nami nilisema: “Unirehemu, ee Yawe,
uniponyeshe, maana nimekukosea.”
6Waadui zangu wanasema hivi vibaya juu yangu:
“Atakufa wakati gani kusudi jina lake lisahauliwe!”
7Wananitembelea bila kuwa na nia njema,
wanawaza mabaya juu yangu,
wanapofika inje wanawatangazia wengine.
8Wote wanaonichukia wananongoneza juu yangu;
wananiwazia mambo mabaya.
9Wanasema: “Magonjwa haya yatamwua;
hatatoka tena ndani ya kitanda chake!”
10Hata rafiki yangu wa moyo niliyemwamini,
rafiki aliyechangia chakula nami,
amegeuka kunishambulia!
11Ee Yawe, unionee huruma!
Uniponyeshe, nami nitawalipiza kisasi.
12Hivyo nitajua kwamba unapendezwa nami,
waadui zangu wasipopata ushindi juu yangu.
13Wewe unaniimarisha katika ukamilifu;
utanichunga mbele yako milele.
14Yawe, Mungu wa Israeli, asifiwe,
tangu milele na hata milele!
Amina! Amina!
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.