1Kwa mukubwa wa waimbaji. Zaburi ya Wakora.
2Musikie jambo hili, enyi watu wote!
Mutege masikio, enyi wakaaji wote wa dunia.
3Musikilize wote, wakubwa na wadogo,
enyi watajiri na wakosefu.
4Maneno yangu ni mazitomazito;
mawazo yangu ni ya hekima.
5Ninatega sikio, nisikilize mezali,
ninafafanua kitendawili kwa muziki wa zeze.
6Kwa nini niogope wakati wa hatari,
wakati ninapozungukwa na uovu wa waadui?
7Watu waovu wanategemea mali zao,
wanajisifia wingi wa utajiri wao.
8Lakini mwanadamu hawezi hata kidogo kujikomboa mwenyewe;
hawezi kumulipa Mungu bei ya maisha yake,
9maana malipo ya ukombozi wa maisha ni kubwa sana.
Hawezi kutoa kitu chochote kinachotosha,
10kimwezeshe aendelee kuishi siku zote,
bila kuona kaburi.
11Inaonekana wazi kuwa hata wenye hekima wanakufa,
nao wapumbafu na wajinga vilevile.
Wote wanawaachia wengine mali zao.
12Ingawa walisema kwamba udongo ni wao,
lakini ni makaburi ndiyo nyumba zao hata milele,
ni makao yao vizazi hata vizazi.
13Mwanadamu hadumu katika utajiri wake;
anakufa tu kama nyama.
14Hayo ndiyo yanayowapata wanaojitumainia kwa upumbafu,
ndio mwisho wa wale wanaojivunia mali zao.
15Wanaongozwa kama kondoo mpaka katika kuzimu;
kifo ndiye muchungaji wao.
Wanashuka moja kwa moja katika kaburi.
Miili yao inaozea huko.
Kuzimu inakuwa makao yao.
16Lakini Mungu atanikomboa kutoka katika kuzimu,
ataniopoa kutoka huko.
17Usihangaike ukiona mutu anatajirika,
wala mali yake ikiongezeka zaidi na zaidi.
18Maana atakapokufa hatachukua kitu chochote,
mali yake haitashuka huko chini pamoja naye.
19Hata akijitukuza katika maisha haya,
na kusifiwa kwa sababu ya kufanikiwa,
20atakwenda kukutana na babu zake waliomutangulia kufa,
ambao hawawezi kuona tena mwangaza.
21Mwanadamu hadumu katika utajiri wake:
anakufa tu kama nyama.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.