1“Ikiwa mwanaume ameoa muke na kisha hapendezwi naye kwa sababu ameona kwake kitu kisichofaa, basi, huyo mwanaume akimwandikia barua ya kuachana, akimupa na kumufukuza kutoka katika nyumba yake, kisha huyo mwanamuke akiondoka,
2na kuolewa na mwanaume mwingine,
3kama huyo mume wa pili akimutwaa, akimwandikia barua ya kuachana, akimupa na kumufukuza toka katika nyumba yake, au kama huyo mume wake akikufa,
4basi, yule mume wa kwanza haruhusiwi tena kumutwaa huyo mwanamuke kuwa muke wake kwa sababu alikwisha kuchafuliwa. Kufanya hivyo ni chukizo kwa Yawe.
5“Mwanaume aliyetoka kuoa asiende kwa vita wala asipewe kazi yoyote ingine; aachwe huru kwa muda wa mwaka mumoja, kusudi akae kwake na kufurahi na muke wake.
6“Mutu yeyote asitwae jiwe la chini au la juu la kusagia kuwa rehani; kufanya hivyo ni kama kutwaa uzima wa mutu huyo.
7“Mutu yeyote akimwiba Mwisraeli mwenzake na kumufanya kuwa mutumwa wake au kumwuzisha katika utumwa, mutu huyo anapaswa kuuawa. Ndivyo mutakavyokomesha uovu kati yenu.
8“Kama mutu akishikwa na ukoma munapaswa kuwa waangalifu kufuata maagizo ya Walawi. Kama vile nilivyowaamuru ndivyo mutakavyofuata kwa uangalifu.
9Mukumbuke jinsi Yawe, Mungu wenu, alivyomutendea Miriamu mulipokuwa katika safari kutoka Misri.
10“Ukimukopesha mwenzako kitu chochote, usiingie kwake kutwaa rehani.
11Usimame inje na umwache yeye mwenyewe akuletee hiyo rehani.
12Kama yeye ni masikini usikae na rehani hiyo usiku kucha.
13Umurudishe kila siku magaribi kusudi usiku aweze kujifunika na kukutakia baraka. Kufanya hivyo ni jambo la uhaki mbele ya Yawe, Mungu wenu.
14“Usimutese mutumishi wako wa mushahara anayekuwa masikini na muhitaji, akuwe Mwisraeli au mumoja wa wageni wanaoishi katika miji yenu.
15Kila siku, mbele jua halijatua, umulipe mushahara wake wa siku hiyo, maana yeye ni masikini na huo mushahara ni tegemeo la moyo wake; kusudi asimulilie Yawe, nawe utakuwa na kosa.
16“Wazazi wasiuawe kwa makosa ya watoto wao, wala watoto wasiuawe kwa ajili ya makosa ya wazazi wao. Kila mutu atauawa kwa makosa yake mwenyewe.
17“Musipotoshe haki za wageni na wayatima. Wala musitwae nguo ya mujane kuwa rehani.
18Mukumbuke kwamba ninyi mulikuwa watumwa katika inchi ya Misri, na Yawe, Mungu wenu, akawakomboa kutoka huko. Kwa hiyo ninawapa amri hiyo.
19“Munapovuna mavuno yenu katika shamba na kusahau masuke mengine humo, musirudi kuyatwaa, lakini muwaachie wageni, wayatima na wajane, kusudi Yawe, Mungu wenu, awabariki katika kazi zenu zote.
20Munapotikisa mizeituni yenu kwa kuvuna matunda, musirudi kutikisa tena vitawi vyake, lakini muwaachie wageni, wayatima na wajane.
21Munapochuma zabibu, musirudi kuokota zabibu zilizobaki lakini muwaachie wageni, wayatima na wajane.
22Mutakumbuka kwamba ninyi mulikuwa watumwa katika inchi ya Misri; kwa hiyo ninawapa ninyi amri hii.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.